Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 14 2023-01-31

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, hadi sasa mpango wa kutatua kero ya maji katika Mji wa Tunduma umefikia hatua gani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha huduma ya upatikanaji ya maji safi na salama inaboreshwa katika Mji wa Tunduma na maeneo yote hapa nchini. Katika Mji wa Tunduma, Serikali inaendelea na upanuzi wa mtandao wa usambazaji maji kilometa10.5 ambapo Kata ya Uwanjani, Tunduma na Makambini zitaanza kupata huduma mwezi Machi, 2023.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali imedhamiria kutekeleza mradi wa kutumia Chanzo cha Mto Bupigi kilichopo katika Wilaya ya Ileje na taratibu za kumpata Mkandarasi zinaendelea na ujenzi wa mradi utaanza kabla ya mwezi Julai, 2023. Mradi huu umepangwa kuhudumia Miji ya Tunduma, Vwawa Mlowo, vijiji 14 vya Ileje na maeneo ambayo bomba kuu litapita. (Makofi)