Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Mradi wa Maji wa Darakuta hadi Minjingu?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninaomba Mheshimiwa Naibu Waziri afanye mawasiliano na wataalam wake wa maji wanaohusika na eneo husika, kwa sababu taarifa anazosema nadhani haziko sahihi na ambazo ninazo. Amesema kazi zinazofanyika labda angesema kazi zitakazofanyika kwa sababu mradi huo kwa sasa umeishia Kata ya Magugu.

Mheshimiwa Spika, la pili; miradi yetu ya maji mingi inachelewa kwa kuwa na utaratibu wa manunuzi ambao huchukua muda mrefu sana.

Sasa Wizara ina mpango gani wa kuboresha kitengo hicho cha manunuzi ili mradi uweze kukamilika kwa wakati? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la kuwasiliana na watendaji naomba nilipokee na nitalifanyia kazi kwa karibu sana kuhakikisha kazi zote zinafanyika kwa wakati kama ambavyo inapaswa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu uboreshwaji wa hatua za manunuzi, Kiwizara tunaendele kuhakikisha tunatumia taratibu ambazo hazitachelewesha miradi na pale itakapobidi basi ushauri tunapokea na tutafanyia kazi. (Makofi)