Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 13 2023-01-31

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza Mradi wa Maji wa Darakuta hadi Minjingu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Darakuta - Magugu ndio unaoendelezwa mpaka Minjingu ambapo utagharimu shilingi bilioni 5.672 na kazi zinazoendelea kufanyika ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu kwenye umbali wa kilometa 46, ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilometa 66, ujenzi wa tanki la lita 250,000 na ufungaji wa pampu. Utekelezaji wa mradi huu umeanza mwezi Septemba, 2022 na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo wananchi wapatao 23,000 wa Kata za Mwada na Nkati watanufaika.