Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Kiangamanka, Ukata, Kipololo na Kijiji cha Kiwombi zitapelekewa mawasiliano ya simu?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongezaa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nitoe masikitiko yangu, Kata ya Ukata haina mnara wa Vodacom. Watu wa Vodacom walikuja wakajenga mnara kata ya Ukata ukakamilika lakini baadae wakauporomosha waliko upeleka hatujui. Pia hiyo minara ya Halotel ya Kata ya Kipololo Kijiji cha Lunoro na kijiji cha Litoho kweli imejengwa lakini haijawashwa tangu mwaka 2017 hadi leo sasa niombe Serikali itueleze itatupa lini mawasiliano katika hivi vijiji nilivyo vitaja?

Mheshimiwa Spika, la pili, Kata hii ya Kihangimahuka iko kilometa 25 kutoka Mbinga Mjini lakini hadi leo haina mawasiliano. Niombe ule mchakato uharakishwe ili wananchi hawa nao wapate mawasiliano, ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, minara hii ilijengwa na inapojengwa baada ya hapo tunafanya technical auditing na baada ya kukamilisha technical auditing maana yake kwamba wanawasha; lakini kuna scenario mbili ambazo huwa zinatokea, ya kwanza wanaweza wakawasha baadaye kukawa na changamoto ya vifaa ambavyo wametumia. Shoti hizo huwa zinatokea lakini baada ya hapo huwa tunatoa maelekezo ya namna ambavyo wanatakiwa kwenda kurekebisha.

Mheshimiwa Spika, changamoto ilikuwepo hapa katikati ni changamoto ya uzalishaji wa vifaa, ambayo tumekuwa nayo kutokana na janga ambalo lilikuwa limetoka katikati. Nchi zote Afrika inawezekana kabisa supplier anakuwa ni yule yule kiasi kwamba tunajikuta tunakuwa kwenye queue ya kusubiri vifaa hivyo viweze kuzalishwa na ili waweze kununua na kulete kwa ajili ya kurekebisha katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, lakini vile vile suala la Kata ya Hukata, ni kweli kabisa nakiri, Kata ya Hukata ambayo nafahamu kabisa ndipo ambapo Mheshimiwa Mbunge anatoka. Nalijua tatizo hili kwa upana huo lakini kilichofanyika ni kwamba baada ya kujenga mnara katika kata ile na scope ya eneo ambalo ilitakiwa kupata mawasiliano haikuwezekana ikabidi tuhamishe mnara uende sehemu nyingine ili kuweza kufikisha mawasiliano katika eneo la Hukata.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyokuwepo; changamoto iliyopo ni kwamba mawasiliano yaliyopo pale kwa sasa bado ni hafifu, kwa hiyo sasa tunaandaa timu yetu iende ikajiridhishe na kuona namna gani sasa tutaenda kulitatua kwa ukubwa wake, ahsante.