Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 11 2023-01-31

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Kata za Kiangamanka, Ukata, Kipololo na Kijiji cha Kiwombi zitapelekewa mawasiliano ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI, alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari na Teknolojia ya Habari napenda kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Kipololo inapata huduma za mawasiliano kutoka kwa Kampuni ya Halotel iliyojenga mnara katika Kijiji cha Lunoro. Kata ya Ukata inapata huduma za mawasiliano kutoka kwa Kampuni ya Vodacom iliyojenga mnara katika Kijiji cha Ukata na vile vile kutoka Halotel iliyojenga mnara katika Kijiji cha Litoho. Minara hii imejengwa kati ya mwaka 2017 na 2019 kwa ruzuku ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kata ya Kiangamanka na Kijiji cha Kiwombi, Serikali itafanyia tathmini ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano kata hii na kijiji hiki Katika mwaka huu wa fedha wa 2022/2023. Tathmini hiyo vile vile itahusisha uhakiki wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yote yaliyopo katika Kata za Ukata na Kipololo, ahsante.