Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti madalali wanaodalalia mazao ya wananchi yakiwa shambani kwa bei wanazozitaka?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kumekuwa na uonevu mkubwa sana na wizi mkubwa wa wananchi wanapoenda kuuza mazao yao sokoni, kuna watu wanaitwa madalali hawa watu ndio wanao panga bei ya mazao na kuondoa fursa ya wakulima kupanga bei ya mazao yao. Je, Serikali ina mpango gani wa kisheria wa kuondoa tatizo hili na kuweza kumlinda mkulima aweze kuuza kwa bei anayotaka yeye?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kumekuwa na changamoto ya uuzaji wa mazao kwa kulazimishwa kuuza kwa rumbesa wakulima wetu. Je, Serikali ni lini itapeleka maagizo maalum kwenye halmashauri zetu za kuzuia uuzaji huu wa rumbesa mazao ya wananchi?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Saashisha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la rumbesa kama alivyojibu Naibu Waziri wa Viwanda hapa mbele ya Bunge lako tukufu vilevile Wizara ya Kilimo tukishirikiana na Wizara ya Viwanda tumeshakuwa na mwongozo rasmi ambao tutaupeleka katika halmashauri zote nchini ili halmashauri waweze kusimamia mwongozo huo kuanzia suala la ununuzi, suala la uwekaji kwenye vifungashio na namna ambavyo mazao yanasafirishwa kwa hiyo hili ni jambo ambalo tutashirikiana pamoja na Serikali za Mitaa kuhakikisha tunalitatua hili tatizo ni kweli lipo na ni tatizo kubwa lakini naamini litakwisha.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hili la madalali walioko masokoni. Kwanza uwepo wa middle man katika biashara ni jamba ambalo limekuwepo toka historia ya Dunia inaumbwa na ni jambo ambalo halikwepeki lakini kuwa na watu wakati ambao hawako regulated hili ndio tatizo ambalo linatukabili kwa hiyo Serikali kupitia Sheria iliyoianzisha Mamlaka ya COPRA hivi karibuni tumeshapeleka mapendekezo atateuliwa Mkurugenzi Mkuu wa COPRA ambaye atakuwa na jukumu la kudhibiti wauzaji na wanunuzi wanaosimamia uuzaji na ununuzi wa mazao katika masoko makuu na masoko ya awali. Kwa hiyo tutaweka utaratibu wa wazi wa kikanuni kwa kufuatana na Sheria ya COPRA ili kuweza kudhibiti na kuhakikisha kwamba mkulima anafaidika na jasho lake.