Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naishukuru Serikali; mwezi Julai mwaka jana tumepokea shilingi milioni 192 kwa ajili ya uendelezaji wa shule hiyo kuwa kidato cha tano na sita. Ni lini Serikali itatuletea fedha kwa ajili ya kukamilisha bwalo na kujenga makataba ya high school?

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa fedha hizi zilikuja zikaanzisha majengo mapya na kuacha yaliyokuwepo. Ni lini Serikali itakamilisha nyumba nne za watumishi zilizopo pale?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tulishaanza hatua ya awali na tumebakisha tu ujenzi wa bwalo pamoja na maktaba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa tutakapopata fedha za mradi ambayo tunayo sasa hivi, tutazitenga kwenye bajeti na kupeleka katika shule hiyo.

Mheshimiwa Spika, na kuhusu majengo mapya ni kwamba kwa sababu sasa hivi tuna miradi mikubwa miwili ya SEQUIP pamoja na BOOST ambapo sehemu ya fedha hizo ni pamoja na kumalizia majengo, kujenga majengo mapya, pamoja na nyumba za walimu. Tutafanya hivi mara tutakapopokea fedha hizo, ahsante.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nipongeze Serikali ya Awamu ya Sita kwa jitihada ya kujenga madarasa katika Jimbo la Buchosa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Jimbo la Buchosa lina kata 21 na watu takribani 400,000 lakini ina high school moja tu. Nilishapeleka maombi Wizarani kwa ajili ya kuomba Shule ya Sekondari Kakobe, Bupandwa na Nyakahilo ziweze kupandishwa hadhi kuwa high school.

Je, Mheshimiwa Waziri, anaweza kutamka wananchi wa buchosa wamsikie ni lini shule hizi zitapandishwa madaraja?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Eric Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mpango tulionao Ofisi ya Rais- TAMISEMI, ni kuziongezea, yaani kwa maana kuzipanua, shule mia moja nchini ili kuzipa hadhi za kidato cha tano na sita kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi iliyoongezeka. Miongoni mwa shule ambayo ipo ni pamoja katika Jimbo la Buchosha. Kwa hiyo nimuhakikishie tu kwamba kuna fedha ambayo tunaisubiria, ikishafika tu tutatekeleza hilo, ahsante sana.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa muda niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nilitaka kuiuliza Serikali, Jimbo la Songwe lina tarafa mbili na kwenye Tarafa ya Kwimba kuna shule moja ya A-level pale Maweni Sekondari, lakini kutoka Maweni Sekondari mpaka ukafike mwishoni kabisa karibu na Ziwa Rukwa kuna Shule ya Sekondari ya Kapalala ambayo ina vigezo vyote vya kuwa na hadhi ya kupata kidato cha tano na imezungukwa na shule sasa takriban nne, Gua Sekondari, Phillipo Mulugo Sekondari, Ngwala Sekondari, na Kapalala yenyewe.

Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi katika shule hiyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la mheshimiwa Phillipo Mulugo, Mbunge wa Jimbo la Songwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa maelezo ya Mheshimiwa Mbunge, aliyoyatoa hapa mimi nimhakikishie kwamba tutatuma wataalamu waende kukagua na kujiridhisha kama vigezo vimetimia ili tuanze mchakato wa kuipandisha hadhi, ahsante sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Shule ya Sekondari ya Mogabili ni shule kongwe na ya bweni ambayo inagharamiwa na wazazi na inachukua wanafunzi wengi sana. Imekidhi vigezo ambavyo vimetajwa na Mheshimiwa Naibu Waziri hapa. Nataka tu kujua kama hii shule ya sekondari itapandishwa hadhi kuwa kidato cha tano na sita katika hizo shule 100 ambazo Waziri amezitaja hapa, anatarajia kuzifanya mwaka huu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba sio shule zote zimeomba kuwa kidato cha tano na sita. Kwa hiyo nitaangalia katika mpango, kama ipo maana yake tutaiweka katika mipango yetu ili iweze kukamilisha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo baada ya kusema maneno hayo naamini Mheshimiwa Mbunge amenielewa.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 5

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Sisi pia kule Namtumbo tuna Shule ya Sekondari ya Sasawala iliyopo katika Tarafa ya Sasawala ambayo iko kilometa 220 kutoka Makao Makuu ya Wilaya na imekidhi vigezo kwa kuwa imeongezwa ina madarasa na mabweni. Tunaomba na sisi tuorodheshwe katika hizo orodha ya Shule za Sekondari 100 kwa kuwa imekidhi vigezo. Je, linawezekana? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Shule imekidhi vigezo jambo hilo linawezekana. Hata hivyo niwathibitishie Wabunge wote kwamba tutapitia maeneo yote ambayo yamekidhi vigezo ili tuweze kuyapa kipaumbele. Ahsante sana.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 6

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, sisi tuliomba tangu mwaka jana kwenye Shule ya Makong’onda hatujajua mpaka sasa hivi hali ikoje?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela, Mbunge wa Masasi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, shule zote ambazo zipo katika maombi ndio tunazifanyia kazi. Tutakapopata hiyo hela maana yake kuna baadhi ya miundombinu ambayo tunatakiwa tukamilishe ili sasa ziweze kupandishwa. Ahsante sana.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 7

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni ukweli usiopingika kwamba Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi imepeleka fedha nyingi sana za kujenga vyumba vya madarasa na sasa watoto wote wanaenda mashuleni. Hata hivyo bado kuna tatizo kubwa sana la nyumba za Walimu. Je, ni lini sasa Serikali itakuja na mkakati thabiti wa kuhakikisha kwamba kunakuiwa na nyumba za Walimu za kutosha ili vijana wetu waweze kusoma vizuri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Vedastus Mathayo Manyinyi, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ndio maana kwa sasa Serikali katika mipango yake kila mahali ambapo tunapeleka shule, tunahakikisha tunajenga na nyumba za Walimu katika kila shule ambayo tunaianzisha. vile vile mikakati mingine tuliyo nayo ni pamoja na kutafuta fedha ili kusogeza huduma hiyo ya makazi kwa Walimu, lakini tumeziagiza halmashauri kutenga fedha katika bajeti zao za ndani kuhakikisha katika kila bajeti ya mwaka wanaweka fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Walimu. Ahsante sana.