Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2023-01-31

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Nghoboko kuwa ya kidato cha tano na sita?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili shule ya sekondari iwe na hadhi ya kidato cha tano na sita inatakiwa iwe na vyumba vya madarasa viwili kwa mkondo mmoja, matundu ya vyoo manne, bweni, maktaba, jiko na bwalo la chakula.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Shule ya Sekondari ya Nghoboko bado haijakidhi vigezo vya kuwa ya kidato cha tano na sita. Kwa kutambua umuhimu wa shule hiyo, Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri inaendelea kutafuta fedha kwa ajili kukamilisha miundombinu ya shule hiyo ili iwe na vigezo vya kupandishwa hadhi na kuwa ya kidato cha tano na sita.