Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Kwanza naishukuru Serikali kwa kuweza kutupatia fedha hiyo na ujenzi unaendelea. Ila sasa kwa kuwa fedha hii inakuja kwa mafungu ya shilingi milioni 500, na kwa kuwa fedha inayotakiwa kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ngara ni shilingi bilioni tatu na zaidi.

Je, Serikali ipo tayari kuongeza muamala kutoka shilingi milioni 500, mpaka shilingi bilioni moja ili tuweze kujenga hospitali yetu kwa wakati na tuimalize? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kupeleka fedha kwenye Halmashauri hii ya Ngara kwa ajili ya ujenzi wa hospitali. Tayari wana bilioni moja; shilingi milioni 500 bado hawajaanza kuitumia. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba mara watakapotumia fedha hiyo kwa wamu ya pili, Mheshimiwa Rais na Serikali yetu itaendelea kupeleka fedha hiyo ili kuhakikisha Hospitali ya Halmashauri ya Ngara inakamilika.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi pia.

Mheshimiwa Spika, tatizo la Ngara ni sawa na tatizo lililoko Biharamulo maana tumeanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya kwa muda mrefu sana, na kuna pesa milioni 204 ilirudishwa, nimeshaiongelea humu zaidi ya mara tano, lakini pia kuna pesa ya bajeti ya mwaka huu milioni 750. Sasa, kwa sababu hospitali hii tumeanza kuitumia tarehe 13 Januari, ila majengo mengine hayajamalizika.

Ni lini mtapeleka pesa hizi ili wananchi wa Biharamulo waweze kutumia Hospitali yao kwa uhuru ili wapate huduma wanayostahili kupata? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kupeleka fedha Biharamilo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri kwa awamu, lakini nafahamu kuna fedha ambazo Mheshimiwa Chiwelesa amekuwa akifuatilia ili kuhakikisha kwamba fedha hizo zinatafutwa, zinapelekwa Biharamulo ili hospitali ile ikamilike ianze kutoa huduma kwa wananchi, ahsante.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 3

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Arusha ina Hospitali ya Wilaya ya Oltrument ambayo tangu Serikali ilipoanza kuboresha Hospitali za Wilaya Hospitali hii haijawahi kukumbukwa hata siku moja.

Je, ni lini Serikali itaona sasa umuhimu wa kuongeza majengo haya katika hospitali hiyo ambayo iliahidiwa na Mheshimiwa Rais tangu mwaka 2012? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah Saputu Molllel, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Arusha inanendelea na ujenzi na ina upungufu wa majengo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kujenga majengo hayo kwa awamu na Hospitali hii pia itapelekewa fedha ili iweze kukamilisha majengo yote muhimu. Ahsante.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 4

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; ni lini Serikali itatenga na kupeleka fedha kwa ajili ya kujenga majengo tisa muhimu ya kutolea huduma za afya katika Hospitali yetu ya Halmashauri ya Handeni Mjini, ili kuipa hadhi iwe sawa na Hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeshapeleka shilingi milioni 900 katika Halmashauri ya Handeni Mjini, kwa ajili ya kuanza upanuzi wa Hospitali hiyo. Nimuhakikishie kwamba zoezi hilo ni endelevu ili tuhakikishe majengo yote tisa yanajengwa na huduma bora zinatolewa kwa wananchi wa Handeni Mjini.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 5

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; hospitali mpya ya Wilaya ya Kwimba iliyoko Icheja ina upungufu mkubwa wa miundombinu ambapo hakuna wodi za Watoto na akina mama na huduma mbalimbali hazipatikani, hivyo kupelekea usumbufu mkubwa kwa wagonjwa kuhitaji kupata huduma katika Hospitali mpya na huduma zingine katika kituo cha afya cha Ngudu, ambapo husababisha gharama kubwa sana za matibabu kwa wagonjwa.

Je, ni lini Serikali sasa itapeleka pesa za kutosha ili kukamilisha huduma za msingi zipatikane katika jengo moja kwenye hospitali mpya ya Icheja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyogeza la Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Jimbo la Sumve kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa hospitali zetu za Halmashauri unakwenda kwa awamu, na kila baada ya awamu majengo kadhaa yanayokamilika yanaanza kutumika na majengo mengine yanapelekewa fedha kwa ajili ya ujenzi na kuanza kutumika. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Halmashauri hii ya Kwimba ni miongoni mwa Halmashauri ambazo zimewekwa kwenye bajeti, kuongezewa fedha ili miundombinu mingine ikamilike kwa ajili ya kutoa huduma, ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 6

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa hospitali yetu ya Wilaya ya Nyang’hwale inaendelea kukamilishwa na Mkurugenzi anatumia lile jengo la utawala.

Je, Serikali inatuambia nini kuhusu kumuhamisha Mkurugenzi huyo ili hospitali hiyo ianze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hospitali imekamilika, lakini kwa sababu ya ukosefu nwa jengo la utawala katika Halmashauri hiyo naomba nilichukue hili tutalifanyia kazi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuhakikishe Hospitali hii sasa inaanza kutoa huduma na isitumike kama jengo la utawala katika Halmashauri hiyo. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya swali la nyongeza.

Kwanza nishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia kwa kutupatia shilingi milioni 900 kwa ajili ya ukarabati wa majengo katika Hospitali yetu ya Wilaya pale Kinyonga, Kilwa Kivinje. Hata hivyo bado hali ya wodi zetu ni mbaya. Serikali ina mpango gani wa kuipatia fedha Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kwa ajili ya kujenga na kukarabati wodi pale Hospitali ya Wilaya Kivinje?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mmheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imekwishakupeleka shilingi milioni 900 ili kiufanya upanuzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa almaarufu Kinyonga; na zoezi hili linakwenda kwa awamu. Baada ya shilingi milioni 900 kutumika na kukamilisha majengo ya awamu ya kwanza Serikali itaendelea kupeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo mengine. Ahsante.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 8

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ilipata shilingi milioni 500; mwaka wa fedha ulipita na mwaka huu wa fedha ilipata shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo mpaka sasa ujenzi huo haujaanza kutokana na kutokuwepo na mawasiliano mazuri kati ya TAMISEMI, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Wizara ya Fedha. Sasa ni lini ujenzi huo utaanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Priscus Tarimo, Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishatoa maelekezo kwamba fedha za miradi ya maendeleo zikiwemo za ujenzi wa hospitali zikishapelekwa katika Halmashauri ujenzi unatakiwa kuanza mara moja ili kupeleka huduma kwa wananchi. Naomba kutumia fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kuhakikisha wanaanza ujenzi wa hospitali hiyo mapema iwezekanavyo ili dhamira ya Serikali ya kuwahudumia wananchi iweze kutimia, ahsante.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Supplementary Question 9

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; naomba kupata maelezo, Hospitali ya Wilaya ya Bunda tumepokea shilingi 3,650,000,000 na haina dalili za kumalizika, na Mheshimiwa Naibu Waziri ulikuja juzi ukaiona. Ni lini itamalizika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imepeleka zaidi ya shilingi 3,200,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda; na wiki mbili zilizopita nilifanya ziara katika Halmashauri hiyo pamoja na Mbunge. Tulikubaliana, kwanza tunachukua hatua za kinidhamu kwa wataalam wote waliosimamia hospitali ile na kupelekea kutokukamilika kwa majengo ilhali fedha zilishapelekwa.

Pili, tumekubaliana kwamba fedha itapelekwa ili ikamilishe majengo yale mapema iwezekanavyo na huduma za afya zianze kutolewa, ahsante.