Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 4 2023-01-31

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ngara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ni miongoni mwa Halmashauri 25 zilizoanza kutekeleza ujezi wa Hospitali kwa awamu ya tatu katika mwaka wa fedha 2021/2022, ambapo ilipokea fedha shilingi milioni 500 na kuanza ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD) na Jengo la Maabara.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Ngara katika mwaka wa fedha 2022/2023 imetengewa fedha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa hospitali. Halmashauri hiyo ilipokea fedha hizo mwezi Novemba 2022 kwa maelekezo ya kutumia fedha hiyo kwa ajili ya ujenzi wa jengo la huduma ya mama na mtoto, pamoja na chumba cha upasuaji wa dharura. Kwa sasa Halmashauri ipo kwenye utaratibu wa kutangaza kazi ili kupata kandarasi ya kusimamia ujenzi, ahsante.