Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatangaza kima cha chini cha mishahara kwa Wafanyakazi wa Serikali na mashirika binafsi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Ahsante kwa majibu yako Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa Mkataba Na. 189 umefikia wapi ili kuboresha mishahara ya wafanyakazi wa majumbani?

Swali langu la pili, suala la kuboresha mishahara ya Wakuu wa Vyuo Vikuu limefikia wapi mpaka sasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari kuhusiana na Mkataba wa Kimataifa Na. 189 tunafahamu kwamba Serikali yetu tayari ilikwisha kuanza kufanyiakazi kwa maagizo ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na kulikuwa kuna vipengele ambavyo bado tulikuwa tunaendelea kuvifanyia kazi kwa maana ya kwamba, vipo ambavyo vinavyoendana na hali yetu ya kiuchumi na uhalisia wa kimazingira pamoja na tamaduni zetu, lakini kuna vifungu vingine ambavyo vilionekana na katika msingi wa Sheria za Kimataifa kuna kusaini Mkataba wa Kimataifa, unaweza uka - ratify lakini pia ukawa una- reservation kwenye baadhi ya maeneo. Kwa hiyo, hizo hatua zote Serikali inaendelea kuzichukua kwa haraka, nina imani ndani ya kipindi cha mwaka huu wa fedha hayo yote tutakuwa tumekwisha kuyaangalia hasa kuhusiana na haki na stahiki za mikataba ya wafanyakazi wa ndani.

Mheshimiwa Spika, katika hilo tumeanza awali kupitia Kamishna wa Kazi kuweza kuona namna gani ambavyo tunaweza kutengeneza standard ambazo zinaendana na nchi yetu za kuangalia maslahi kwenye kundi hili ambalo kimsingi maeneo mengi wanakuwa na uonevu na manyanyaso mengi. Kwa hiyo, tunaliangalia sana kama Serikali.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la Mheshimiwa Medard Ntara ni kuhusu maboresho ya mishahara katika Vyuo Vikuu. Hili tayari limeanza kufanyiwa kazi na Ofisi ya Waziri Mkuu ambaye ni mratibu na Wizara ya Elimu ambayo pia ndiyo yenye dhamana hii katika kuangalia. Tunazidi kuangalia viwango kulingana na hali ya kiuchumi, pia uhalisia wa kidunia kwa sasa. Kwa hiyo, hivi karibuni Mheshimiwa Ntara nitamueleza hatua ambazo tumekwisha kuzifikia. Kwa hatua ya sasa siyo vema sana kuzitaja hapa hadharani. Ahsante. (Makofi)