Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama hapa kwa mara ya saba kulalamikia uwanja wa Sumbawanga Mjini, leo nataka commitment ya Serikali, ni lini kazi ya ujenzi wa uwanja wa Sumbawanga Mjini utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali sasa ina mpango gani wa kuweka basi hata route ya kutoka Songwe moja kwa moja mpaka Dodoma wakati huo inaendelea kujipanga kwa ujenzi wa Sumbawanga Mjini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, ilitakiwa kiwanja hiki kianze kujengwa mwaka wa fedha wa 2017/2018, lakini kutokana na changamoto ambayo ilikuwepo EIB hawakutoa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mbunge amenisikiliza tayari EIB wameshatoa Dola Milioni 12 kwa ajili ya kuanza viwanja hivi vinne. Lakini kwa kuwa usanifu ulifanyika zamani, Mkandarasi ameomba mkataba huo urudiwe kwa sababu ya gharama, na kwa sababu gharama zitabadilika lazima tuwasiliane na mtoa fedha ili aweze kutoa no objection.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu nimesema kama atatoa kwa sababu Mkandarasi yupo basi itaanza kujengwa kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu route ya Songwe hadi Dodoma, tumelichukua lakini pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Shirika letu la Ndege la ATCL inayafanyia kazi masuala yote haya ya usafiri kuona namna ya kuunganisha kati ya Dodoma - Mwanza, Dodoma- Kilimanjaro, Dodoma – Mbeya, lakini hii itategemea na wao watakavyofanya study kuona kama wakifanya hivyo kwao biashara itakuwa ni nzuri. Kwa hiyo, wapo wanaendelea kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Kwa kuwa hii ni Wizara ya Ujenzi, Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini TANROAD wataenda kutengeneza barabara ambayo wameiparua pale Kata ya Segerea kwa muda wa Miezi Mitatu sasa na wananchi wanapata vumbi. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kalua Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hii barabara imekuwa inatengenezwa kwa vipande na kipande anachokisema kweli tulikuwa tumeanza kufanya maandalizi lakini kulikuwa na shida ya kupata msamaha wa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba msamaha huu umeshatolewa na mara moja Mkandarasi atakuwa yuko site kuondoa lile vumbi ambalo linaleta shida kwa wananchi wa Jimbo la Segerea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba tu kupitia nafasi hii pia nimjulishe ama kumuagiza Meneja wa TANROADS kwamba kwa kuwa msamaha umeshatolewa basi Mkandarasi aende site ili aweze kukamilisha kazi ambayo anatakiwa aifanye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, uwanja wa ndege wa Ruganzo umejengwa muda mrefu umechoka na sasa unahitaji ukarabati. Na kwa kuwa, sasa Ngara imefunguka, wageni ni wengi, Nickel inatakiwa kuchimbwa na biashara mpakani imeshamiri.

Je, ni lini Serikali itakuja kukarabati uwanja wa ndege wa Ruganzo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala lake limepokelewa na tunajua wageni wengi wanaenda Ngara ambapo ni mbali kutoka viwanja vyote vya ndege ambavyo viko karibu. Kwa hiyo, suala lake tumelichukua na Serikali itatafuta fedha ili kuweza kukikarabati kiwanja hiki ili wageni na watu mbalimbali waweze kufika kwa urahisi kwa ndege katika Wilaya ya Ngara.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Naibu Waziri anajibu swali la msingi, alitaja viwanja Vinne lakini kwa bahati mbaya kiwanja cha Tanga sijakiona ilihali Tanga tuna ujenzi wa bomba la mafuta na ujenzi huu utahitaji uwanja wa ndege wa Tanga uwe umepanuliwa kwa ajili ya kutoa huduma.

Je, ni upi mkakati wa Serikali kupanua uwanja wa ndege wa Tanga ili kuruhusu shughuli za bomba la mafuta?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja nilivyovitaja vine vipo kwenye package moja, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Shangazi kwamba Serikali kama bajeti ya mwaka huu tunaokwenda kuipitisha itapita, kuna viwanja vingine ambavyo pia tuna mpango wa kuvipanua na hasa kiwanja alichokisema cha Tanga ambacho katika kipindi hiki ni kiwanja muhimu sana kwa shughuli ambazo zinaendelea katika Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuna uwanja wa Tanza, kuna uwanja wa Lake Manyara, Simiyu, Lindi, ni kati ya viwanja ambavyo tunategemea kama bajeti itapita, vitakuwa ni baadhi ya viwanja ambavyo tutavipanua na kuvifanyia maboresho makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mkoa wa Simiyu upo kwenye Ilani na eneo tayari limeshajengwa.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa ndege katika Mkoa wa Simiyu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyomjibu Mheshimiwa Shangazi, nimetaja kiwanja cha Simiyu kwamba ni kati ya viwanja ambavyo vipo katika bajeti ambayo tunaenda kwenye mpango wa kuanza kivijenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa Njombe Mjini ni uwanja ambao wananchi wanauhitaji mkubwa sana wa usafiri wa anga, na kwenye ahadi ya Chama cha Mapinduzi umesemwa, Waziri Mkuu ameahidi.

Je, ni lini sasa uwanja huo utaanza ujenzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli uwanja wa Njombe unatakiwa ujengwe na tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika. Serikali inatafuta fedha ili iweze kufanya usanifu wa kina wa uwanja huu ili uweze kujengwa hasa tukizingatia kwamba nguvu kubwa ya kiuchumi ya Mkoa wa Njombe, kwamba tunahitaji kuwa na uwanja kwa ajili ya ku-attract si tu wafanyabiashara, lakini pia tunajua ndiyo kuna uwekezaji mkubwa wa madini ya makaa ya mawe na chuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuna uhakika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha kufanya usanifu na hatimae kuujenga huo uwanja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.