Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 47 2022-04-12

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango wa kukamilisha ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga ni miongoni mwa miradi ya Ujenzi na Upanuzi wa Viwanja vya Ndege Vinne (4) ambavyo ni Kigoma, Tabora, Sumbawanga na Shinyanga inayotarajiwa kutekelezwa kwa Ufadhili wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank - EIB).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa, matakwa ya kimkataba kati ya Serikali na EIB yamekamilishwa na mfadhili tayari ameshatoa fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi huu ulichelewa kuanza kwa wakati, kwa sasa taratibu za kimkataba kati ya Serikali na Mkandarasi zinaendelea. Aidha, Mkandarasi amewasilisha maombi ya kufanyika kwa marekebisho ya Mkataba wa awali. Hivyo, marekebisho haya yameshafanyika na kuwasilishwa kwa Mfadhili (EIB) kwa ajili ya kupata idhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa, Serikali imejipanga kuanza utekelezaji wa mradi huu kabla ya mwaka wa fedha 2021/2022 haujaisha endapo idhini itatolewa na mfadhili kwa wakati.