Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuunganisha mifumo ya Kitambulisho cha Mpiga Kura na Kitambulisho cha Taifa ili kuepusha usumbufu kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Pamoja na majibu mazuri ya Mhehimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kitambulisho cha NIDA kinamthibitisha mtu kwamba ni Mtanzania, inakuwaje sasa wakati mtu anakwenda kutafuta hati ya kusafiria (Passport), anaombwa vitu vilevile alivyokuwa anaombwa wakati anaomba hati ya kusafiria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Je, Serikali haioni sasa umuhimu wa kufanya hiyo namba ya Kitambulisho cha Taifa kuwa hiyo hiyo namba ya TIN na kuwa hiyo hiyo namba ya mita ya umeme kwa watu ambao wana nyumba zao? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali la Mheshimiwa Dkt. Askofu Josephat Gwajima maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapofika wakati tukawa tuna mdadisi mtu mara mbilimbili maana yake tumemdadisi kwenye NIDA pia tunamdadisi tupate maelezo yake kwenye hati ya kusafiria, suala kubwa hapa tunataka tujiridhishe. Kwa hiyo inabidi lazima tufike wakati tumhoji ili tuweze kujiridhisha kwa sababu hali za mifumo zinabadilika lakini na hali za binadamu pia zinabadilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana kitambulisho ambacho alikuwa nacho, kwa sababu vitambulisho pia vina-expire date, vinakuwa na date of issue, kwa hiyo tunataka tujiridhishe kwamba ni yeye na labda alipotokea na mazingira mengine, kwa hiyo, kubwa hapa huwa tunataka kujiridhisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lake la pili ameuliza Je, Serikali haioni haja ya kusema sasa tuunganishe mifumo. Hilo ni jambo jema na tunalichukua ni wazo zuri kwenda kulifanyia kazi kwa sababu siyo Tanzania tu, zipo nchi ambazo tayari zimeshafanya huo mfumo na zinatumia NIDA na kitambulisho kingine. (Makofi)