Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 43 2022-04-12

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuunganisha mifumo ya Kitambulisho cha Mpiga Kura na Kitambulisho cha Taifa ili kuepusha usumbufu kwa wananchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuunganisha mifumo ya Kitambulisho cha Mpiga Kura na Kitambulisho cha Taifa ili kutumia Kitambulisho cha Taifa katika uchaguzi wa kawaida na ule wa kieletroniki (e- voting).

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi haya yatapunguza gharama kwa Serikali katika kuandikisha na kutengeneza daftari pamoja na kurahisisha usimamizi wa wapiga kura.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano kati ya Taasisi hizi mbili yenye dhumuni la kuwezesha kanzidata ya NIDA kutumika katika katika zoezi la uboreshaji wa daftari la Wapiga Kura yameanza mwezi Machi, 2022. Mazungumzo ya awali kati ya wataalam wa taasisi zote mbili yenye nia ya kuunganisha mifumo hiyo miwili yamepangwa kufanyika kabla ya mwezi Mei, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matarajio ya Serikali ni kuona mifumo hiyo inaunganishwa ili kuwarahisishia wananchi kushiriki katika shughuli za uchaguzi na kuipunguzia Serikali gharama katika uandikishaji na uchapishaji wa vitambulisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.(Makofi)