Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na uharibifu unaotokana na ukataji mikoko na uvunaji wa matumbawe ili kuvinusuru visiwa visitoweke?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza ni kwamba pamoja na juhudi kubwa za Serikali za kuangalia hifadhi ya mazingira lakini swali la kwanza ni kwamba Serikali ina mpango gani wa kuviwezesha vikundi vinavyojishughulisha na upandaji wa mikoko pamoja na matumbawe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika visiwa vidogovidogo vilivyopo Pemba Kisiwa cha Mtambwi Mkuu ni moja kati ya visiwa ambavyo vinaathirika kwa hali ya juu kabisa.

Je, Serikali ina mpango gani kukihami kisiwa kile ili kisipotee katika sura ya dunia? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA
MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Ali Omar, Mbunge wa Wete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Omar kwa kazi nzuri anayoifanya kutuwakilisha katika suala zima la utunzaji na uhifadhi wa mazingira hasa katika suala la uhifadhi wa vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo juhudi mbalimbali ambazo tumezichukua katika kuhakikisha kwamba tunawasaidia hawa watu wa vikundi, cha kwanza ni kuelimisha. Tumegundua kwamba changamoto kubwa iliyokuwepo ni kwamba watu wengi taaluma kwao imekuwa ni changamoto. Kwa hiyo, tumekuwa tukichukua juhudi ya kuwaelimisha kuhusu suala la uhifadhi wa mazingira pia tunawahamasisha juu ya upandaji wa miti na kuishughulikia, kwa sababu kuipanda ni suala moja na kuishughulikia ni suala jingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nitoe wito kwa jamii hasa Waheshimiwa Wabunge tushirikiane, kila mmoja apande mti lakini kila mtu ashughulikie mti wake, kuipanda tu miti haitoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa zaidi kwa kushirikiana na Wizara ya Uvuvi tunahakikisha kwamba tunapambana dhidi ya uvuvi haramu ambao unaharibu hayo masuala ya mazingira.

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na uharibifu unaotokana na ukataji mikoko na uvunaji wa matumbawe ili kuvinusuru visiwa visitoweke?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa Vijiji ambavyo vipo hatarini kutoweka kwa miamba hii ya matumbawe ni Kijiji cha Pwani Mchangani ambacho kipo katika Jimbo langu la Chaani.

Je, ni lini Serikali itachukua hatua za haraka ili sasa kunusuru Matumbawe yale yasiharibike lakini pia yasitoweke kutokana na shughuli za kibinadamu ambazo zinaendelea?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Juma Usonge Mbunge wa Jimbo la Chaani Kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nae nimshukuru na nimpongeze kwamba ni mmoja wa miongoni mwa Mabalozi wetu wazuri wa mazingira hasa katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo juhudi mbalimbali ambazo tumepanga kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Kijiji cha Pwani Mchangani kinaendelea kuwa salama hasa katika suala zima la uhifadhi wa mazingira. Moja ni kupitia taaluma lakini yapo matumbawe ambayo tumeshayaandaa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakwenda kuyaweka angalau sasa vile viumbe ambavyo vimo kwenye bahari viweze kuishi katika mazingira ambayo wanaweza waka-survive ili waweze kuhifadhi mazingira zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)