Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga njia mbili katika barabara ya Bandarini hadi Rwamishenye na CRDB mpaka Njiapanda ya Kashai ili kuondoa msongamano?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza.

Ili kuweka taarifa sahihi kwa wananchi wangu wa Bukoba Mjini. Je, Serikali kupitia TARURA ina maana kuwa barabara hizi zimehamishiwa TARURA badala ya TANROADS nilitaka kujua hilo maana hizi barabara ni za TANROADS siyo za TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kumekuwepo na malalamiko mengi ya fidia kwenye miradi ya aina hii. Je, Serikali inatoa ahadi gani kwa wananchi wangu wa Bukoba Mjini endapo wakipitiwa katika hii barabara watapata fidia kwa uharaka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba anasema barabara hii huenda imehamishwa kutoka TANROADS kwenda TARURA, nimwambie tu kwamba hapana ni kwa sababu Serikali hii ni moja na inafanya kazi kwa pamoja nasi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia TARURA na TANROADS tunafanya kazi kwa umoja. Kwa hiyo, kikubwa katika swali lake la msingi alilouliza hapa juu ya kuhakikisha usanifu unakamilika na ujenzi wa barabara unaanza vitafanyika kama ambavyo ameainisha hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kuhusu fidia anataka tu mara baada ya usanifu ni wananchi wale walipwe fidia kwa wakati, Serikali italipa fidia kulingana na tathmini ambayo itafanywa katika maeneo hayo. (Makofi)