Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2022-04-12

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga njia mbili katika barabara ya Bandarini hadi Rwamishenye na CRDB mpaka Njiapanda ya Kashai ili kuondoa msongamano?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Bandarini – Rwamishenye yenye urefu wa kilomita 4.6 inafanyiwa usanifu wa kina ulioanza tarehe 22 Machi, 2022 kwa ajili ya kuwa Barabara ya njia mbili. Kazi ya usanifu inafanywa na Mhandisi Mshauri Luptan Consult Ltd kwa gharama ya Shilingi Milioni 70.05 na kazi inategemewa kukamilika mwezi Mei, 2022. Kazi za ujenzi zitaanza mara baada ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usanifu wa barabara ya CRDB – Njiapanda ya Kashai yenye urefu wa kilomita 0.5 itaanza mara tu kazi ya usanifu wa kina wa barabara ya Bandarini – Rwamishenye utakapokamilika na fedha za usanifu zitakapopatikana.