Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiweke ulazima wa hitaji la kisheria kuwa Taxpayer Tax Audit ifanyike kila mwaka badala ya kusubiri miaka mitatu?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru Serikali kwa majibu yake lakini nikiangalia majibu haya naona kana kwamba yanakinzana na azma ya blue print ambayo inataka wafanyabiashara kwa maana ya walipa kodi waweze kufanya biashara zao wa urahisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Siku zote ukaguzi husababisha interest na penalties kitu ambacho kinafanya ulipaji wa kodi ule unakuwa mgumu. Kuna ukakasi gani kwa Serikali kuweza kuleta mabadiliko kwamba tax audit sasa zifanyike kila mwaka?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuchelewesha hizi tax audit wafanyabiashara wanabambikiziwa makodi makubwa sana kiasi kwamba wanakimbilia kwenda mahakamani, fedha za Serikali hazikusanywi inavyopaswa na kwa wakati. CAG anazungumza trillions of moneys zimekwama kule katika mahakama. Hivi Serikali haioni kwamba ni wakati sasa kurahisisha shughuli za ukokotoaji wa kodi ili fedha za Serikali ziweze zikapatikana kwa urahisi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza tunalichukua kama ushauri, Serikali itaenda kufanya utafiti tukiona kwamba umuhimu wa kuwekwa sheria hiyo basi Bunge lako tukufu tutapeleka mapendekezo yetu na kutunga sheria nyingine ambayo tufanye ukaguzi wa kila mwaka kwa wafanyabiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili pia nalo tunaenda kulifanyia ukaguzi na utafiti kama kweli fedha zinapotea basi atatusaidia na Wabunge wenzangu atatusaidia namna gani ya kuweza kudhibiti na kukusanya fedha hizo kwa wakati stahiki. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiweke ulazima wa hitaji la kisheria kuwa Taxpayer Tax Audit ifanyike kila mwaka badala ya kusubiri miaka mitatu?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nchi yoyote ambayo inahitaji kukusanya mapato kwa wingi na kuwatengenezea mazingira mazuri wananchi wake wamekuwa wakiweka mazingira mazuri ya kodi yaani kodi zinakuwa rafiki si kubwa kulingana na biashara ya mtu anayoifanya. Lakini hapa katikati kodi zimekuwa kubwa kulingana na biashara ya Watanzania wanazozifanya na kumekuwa na malalamiko mengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali inamkakati gani wa kuweka kodi rafiki ili mtanzania ajivunuie kulipa kodi ili kuchangia maendeleo katika Taifa lake?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeandaa mazingira rafiki ya ulipaji kodi isipokuwa baadhi ya wafanyabiashara wanakuwa ni wababaishaji katika biashara zao baadhi yao, lakini nalo niseme kwamba tunalichukua kwenda kulifanyia kazi.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiweke ulazima wa hitaji la kisheria kuwa Taxpayer Tax Audit ifanyike kila mwaka badala ya kusubiri miaka mitatu?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la Mheshimiwa Tarimba lilisema Serikali inachukua muda mrefu wa kufanya Tax Audit matokeo yake watu wanabambikiziwa kodi kubwa. Waziri umesema unataka ukafanye utafiti, CAG ameainisha kwamba kuna kesi za kikodi zenye thamani ya zaidi ya trilioni 350…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Halima uliza swali lako.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, trilioni 350 zimekwama kwa sababu ya kesi za kikodi. Unahitaji kufanya utafiti gani zaidi juu ya suala la Mheshimiwa Tarimba ni muhimu? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tuliposema kufanya utafiti lazima tujiridhishe na kama kesi zipo mahakamani tunaiachia mahakama ifanye shughuli zake.