Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 7 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 62 2022-04-14

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isiweke ulazima wa hitaji la kisheria kuwa Taxpayer Tax Audit ifanyike kila mwaka badala ya kusubiri miaka mitatu?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Usimamizi wa Kodi, Sura 438 kifungu cha 45 imeainisha mamlaka ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kufanya ukaguzi au uchunguzi wa masuala ya kodi kwa walipakodi wote, wakati wowote na sio kwa kuzingatia muda wa miaka mitatu isipokuwa ni pale tu inapoonekana kuna viashiria vya upotevu wa mapato ya Serikali ili kukomboa kodi ambayo haijakusanywa.

Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa viashiria hivyo ni Pamoja na: -Mwenendo usioridhisha wa ulipaji kodi; Mlipakodi kutokufuata Sheria za kodi; aina ya biashara au shughuli ya kiuchumi anayofanya mlipakodi husika; na suala lingine lolote ambalo Kamishna Mkuu ataona ni muhimu ili kuhakikisha kuwa kodi stahiki inakusanywa.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kulitaarifu Bunge lako tukufu kuwa ili kupunguza ulazima wa Kamishna Mkuu kufanya uchunguzi na ukaguzi wa mara kwa mara kwa walipa kodi ni muhimu walipakodi wote kuzingatia matakwa ya sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya kodi iliyopo. (Makofi)