Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli majibu ya Naibu Waziri yananifikirisha sana. Mfadhili ameshapatikana, fedha zimeshatolewa, mkataba umesainiwa mwaka 2017 na wameomba price adjustment. (Makofi)

Je, ni lini Serikali itaongeza hizo fedha ili kazi ianze?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Naibu Waziri amesema kwamba ujenzi utaanza endapo mkandarasi atawasilisha hati ya dhamana ya malipo; ni nini kauli ya Serikali endapo mkandarasi hatawasilisha kwa wakati kama alivyosema kwenye jibu lake la msingi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, price adjustment haizuii uwanja kuanza, lakini ni utaratibu kwa kuwa mkataba ulikuwa wa zamani lazima tuwajulishe hawa wafadhili kwamba kutakuwa na ongezeko la bei na endapo pia hawatataka kuongeza Serikali itaendelea kujenga huu uwanja kwa ile nyongeza ambayo itakuwepo kwani tayari wameshatoa milioni 12 United States dollars kwa ajili ya kuanza ujenzi wa viwanja hivyo.

Mheshimiwa Naibu spika, na hati ya dhamana ni kwamba tayari mkandarasi yuko tayari kuanza kujenga na sasa hivi anachofanya tu ni kuandaa hizo hati ili aweze kuziwasilisha baada ya hiyo fedha kutolewa na wafadhili, ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana ni Asia Halamga, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Naibu Waziri amewahi kuja kukagua eneo la ujenzi wa uwanja wa ndege lililopo kata ya Mwada eneo lenye takribani ya hekari 600 na halina mgogoro wowote.

Je, ni lini Serikali sasa italeta fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mkoa wa Manyara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli uwanja huu utajengwa eneo linaloitwa Mwaga na sasa hivi tunavyoendelea ni kwamba tuko kwenye hatua ya utwaaji wa eneo hilo na pia lilikuwa ni agizo la Mheshimiwa Makamu wa Rais wakati anafungua daraja la Magala kwamba kazi hiyo ifanyike haraka. Kwa hiyo Serikali tuko tunaendelea kulifanyia kazi tuweze kutoa na kuwalipa fidia halafu ujenzi uanze.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge hili kwa bajeti inayoendelea inayoishia Juni, 2022, ilipitisha kwamba kiwanja cha ndege cha Kilwa Masoko kifanyiwe ukarabati na maboresho, mpaka tunazungumza kazi iliyofanyika ni ya kilometa moja kwa kiwango cha changarawe bado mita 950.

Nini maelezo ya Serikali kuhusiana na mita 950 zilizobaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge Mbunge wa Kilwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali ilivyoahidi tumeshakamilisha kilometa moja na tutaendelea kuzikamilisha hizo kilomita 900 zilizobaki kwa kiwango cha changarawe ili tuweze kutimiza ile ahadi ambayo tuliahidi kuifanya, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kigoma ni lango kuu la uchumi wa nchi yetu kwa sababu umepakana na nchi za jirani za DRC Congo na Burundi. Mara nyingi serikaliimekuwa ikiahidi kuja kujenga uwanja wa ndege Kigoma na kuweka taa kwa maaa ya ndege ziweze kuruka usiku.

Sasa nataka Waziri aniambie ni lini Serikali itakuja kuweka taa na kuongeza uwanja wa ndege wa Mkoa wa Kigoma kwa sababu Kigoma imepakana na nchi jirani za Congo na Burundi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kigoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanja cha Kigoma ni kati ya viwanja vinne ambavyo ni Kigoma, Tabora, Sumbawanga na Shinyanga ambavyo vinafadhiliwa na European Investment Bank na ni kati ya viwanja ambavyo tayari fedha imeshatolewa na moja ya kazi ambayo fedha hii inaenda kufanya ni kujenga uzio, jengo la abiria, runway ikiwa ni pamoja na kuweka taa ili kiwanja hiki kiweze kufanya kazi saa 24.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tayari Serikali inaenda kujenga huu uwanja kama ulivyosema. Ahsante.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 5

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante uwanja wa ndege Mkoa wa Njombe haupo kabisa kwenye utekelezaji wa bajeti uliopita na hata bajeti iliyopo ya sasa, lakini kwenye ilani umekuwa ukiutaja kama ni moja kati ya viwanja mnaenda kuvitenga.

Wananjombe wanauliza ni upi mkakati wa Serikali kujenga uwanja wa ndege Mkoa wa Njombe kwa sababu uwekezaji wa parachichi na mambo mengine sasa hivi wanauhitaji mkubwa, lakini wananjombe walioko nje wengi matajiri wanahitaji kusafiri kupitia ndege kurudi Njombe ni upi mkakati wa Serikali?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nikweli kwamba uwanja wa Njombe ni muhimu na eneo lipo tayari. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itakapopata fedha na hasa kulingana na umuhimu wa uwanja huo tutaanza kufanya kwanza utwaaji na kulipa fidia lakini pia kuanza usanifu wa kina, lakini hili Mheshimiwa Mbunge itategemea na upatikanaji wa fedha na utekelezaji wa ilani ni wa miaka mitano. Kwa hiyo nikuhakikishie kwamba hata kama kwa sasa hatujaanza kutekeleza lakini utatekelezwa katika miaka hii mitano, ahsante.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 6

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Singida uko karibu sana na Makao Makuu ya nchi Dodoma na kwa sababu ya kiusalama uwanja wa ndege wa Singida ni muhimu sana na kwa sababu Marais wote wawili wametaja kwenye hotuba zao hapa Bungeni Rais John Pombe Magufuli pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan walisema katika viwanja 11 na kiwanja cha Singida kitajengwa.

Sasa naomba nijue ni lini sasa Serikali itatenga fedha ili kujenga uwanja ule ambao upo karibu na Makao Makuu ya nchi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu, Mbunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, maelezo ya Mheshimiwa Mbunge ni sahihi na ni kweli kwamba viongozi wameahidi uwanja huu uweze kujengwa na mimi naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara tayari ina mpango wa kuanza kufanya tathmini ya uwanja huu ili iweze kuujenga lakini pia kama ulivyosema ni uwanja ambao upo karibu na Dodoma kwa ajili ya usalama. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hilo Wizara inalo na muda si mrefu itaanza kulifanyia kazi, ahsante.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza ni lini uwanja wa Mbeya utaanza kutumika usiku na mchana?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe, Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyoongea uwekaji wa taa kwa uwanja wa Mbeya ambao ni Songwe airport upo pengine kwenye asilimia 95 uwekaji wa taa, runway imeshakamilika zaidi ya mita 3000, uzio na sasa hivi tunakamilisha pia jengo la kisasa la abiria. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba uwanja huu utaanza kutumika, taa zimeshajengwa na utaanza kupokea ndege usiku na mchana ili kuhakikisha kwamba uwanja huo unatumika kwa asilimia 100, ahsante.