Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 61 2022-04-14

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga kama ilivyoanishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mhe. Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga ni miongoni mwa miradi ya ujenzi na upanuzi wa viwanja vya ndege vinne ambavyo ni Kigoma, Tabora, Sumbawanga na Shinyanga inayotarajiwa kutekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank - EIB).

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa matakwa ya kimkataba kati ya Serikali na EIB yamekamilishwa na mfadhili tayari ameshatoa fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi hii. Aidha, Mhandisi Mshauri pamoja na mkandarasi wameonesha utayari wa kuanza kazi na mikataba kati yao na Serikali ilishasainiwa tangu mwaka 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi huu umechelewa kuanza kwa wakati, Mhandisi Mshauri pamoja na mkandarasi wameomba ongezeko la fedha katika kipengele cha price adjustment ili kuweza kuendana na mabadiliko ya bei ya bidhaa kwa soko la sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga kuanza utekelezaji wa mradi huu kabla ya mwaka wa fedha 2021/2022 haujaisha, nah ii itatokana na endapo mkandarasi atawasilisha hati ya dhamana ya malipo ya awali kwa wakati. Ahsante.