Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na nia nzuri ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na wingi wa abiria wanaotumia uwanja wa ndege wa Bukoba na kutokana na ufinyu na huduma hafifu za uwanja wa ndege wa Bukoba. Uwanja wa Bukoba mwaka 2020 tulipokea abiria zaidi ya 44,000 na mwaka 2021 tumepokea abiria 45,000.

Je, Serikali haioni kuna uharaka wa kujenga Uwanja wa Ndege wa Omukajunguti?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika majibu ya Serikali imesema wamefanya tathmini ya kulipa watu watakaopisha ujenzi wa uwanja huo.

Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wakazi wa eneo lile wa Mkajunguti ili waweze kupisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Omukajunguti? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na idadi kubwa ya abiria ambao ndio wanatumia uwanja wa Bukoba ndiyo maana Serikali imeamua kwamba kuna haja ya kujenga uwanja mkubwa zaidi kwa sababu uwanja wa Bukoba kwa mahali ulipo hauwezi kuendelezwa kwa maana ya kuipanua na ndio maana Serikali imetafuta eneo jipya ambalo uwanja mkubwa unaweza kujengwa ili kuruhusu ndege kubwa hasa tukizingatia umuhimu wa uwanja huo na abiria walivyo wengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la fidia, Serikali ilishafanya tathmini ya awali ambayo kwa mujibu wa fidia hatuwezi kuitumia tulifanya tathimini ilikuwa inaenda kwenye bilioni tisa. Kwa hiyo, kuna utaratibu tunaufanya tuweze kurudia ile tathmini twende na hali ya sasa na mara tutakapokamilisha basi fidia italipwa kabla ya kuanza ujenzi wa uwanja huo wa ndege wa Omkajunguti. Ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru; kwenye Wizara hiyo hiyo ya Ujenzi na Uchukuzi tuna changamoto kubwa sana ya barabara ya Mafinga – Mgololo na Nyororo – Mtangwo ambazo zimeahidiwa kuanzia Serikali Awamu ya Nne mpaka Awamu ya Tano, na tarehe 26 Aprili, 2021 Serikali Awamu ya Sita imetoa commitment letter kuanza kujenga barabara hizo.

Nataka kujua ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi hii ya kuwajengea barabara wananchi Mufindi Kusini ili waweze kunufaika na barabara hizo? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliamuahidi Mheshimiwa Mbunge na ni ahadi ya viongozi wa Kitaifa tangu Awamu ya Kwanza kwamba barabara hii ambayo ni barabara kuu lakini ni barabara kimkakati kwamba tutaijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge endapo bajeti ambayo tunaenda kuipitisha itapitishwa bila mabadiliko, barabara hii imeweza kuwekwa kwenye mpango ili iweze kujengwa kwa kiwango lami hasa tukizingatia kwamba sehemu kubwa ya mazao ya mbao tunayoyaona Tanzania yanatoka katika eneo hilo.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 3

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, naomba niende moja kwa moja kwenye swali langu dogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na uwepo wa viwanja vya ndege gharama au nauli za ndege zimekuwa juu sana nini kauliya Serikali kuhusiana na kuhakikisha nauli hizi zinakuwa himilivu kwa Watanzania hasa baada ya kuwa wamehamasika sana?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la nauli ni suala la kibiashara na nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wenzetu wa ATCL kuna taratibu ukifanya booking mapema bei inashuka lakini kama utanunua tiketi utaratibu wa mashirika mengi ya ndege kama utachelewa kununua tiketi ya ndege siku zote bei inakuwa juu, lakini kama utafanya booking mapema basi nauli inakuwa ni ya chini.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 4

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kuuliza Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inakamilisha uwanja wa ndege wa Songwe kwa kuweka vifaa vya kupoozea mazao yaani cold rooms ili kusudi wananchi wa Wilaya ya Mbozi na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini waweze kuhakikisha kwamba wanasafirisha maparachichi na matunda mengine?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uwanja wa ndege wa Songwe sasa hivi tuko kwenye kukamilisha kuufanya kuwa kati ya viwanja vikubwa vya Tanzania vya ndege ambapo kutakuwa na uwezo wa kupokea ndege zote kubwa zinazoruka katika Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hatua ya pili ni kujenga storage facility zikiwepo na hizo za kutunza vifaa ambavyo ni baridi kwa ajili ya kusafirisha nje na ndio maana Serikali ina mpango tayari wa kununua ndege ya kusafirisha mizigo. Kitu cha kufanya ni kujenga hizo storage facility ikiwepo Mkoa wa Mbeya, ahsante.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 5

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, barabara ya Buramba – Bunda - Nyamuswa inayotekelezwa kwa kiwango cha lami wananchi wamebomolewa nyumba zao pale. Ni lini Serikali itawalipa fidia yao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maboto Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini ilishafanyika, wananchi walishaainishwa na sasa hivi Serikali inafanya kupitia yale malipo ili waweze kulipa fidia hiyo.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Supplementary Question 6

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, licha ya juhudu za Serikali za kuendelea kukarabati viwanja wa ndege bado vingi vimekuwa vinafanya kazi mchana tu. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha viwanja vinafanya kazi saa 24?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi viwanja vyote tunapoongelea kiwanja cha Mbeya, kiwanja cha Songwe, kiwanja cha Mtwara, kiwanja cha Msalato, kiwanja cha Geita na hata hivyo viwanja vile tunavyojenga Sumbawanga, Kigoma, Tabora na Shinyanga vyote viko kwenye mpango wa kujengewa taa ili viweze kufanya kazi saa 24 na kazi hiyo inaendelea. Ahsante.