Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 60 2022-04-14

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Omukajunguti ili kuruhusu ndege kubwa kutua Bukoba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa kujenga kiwanja kipya cha ndege katika eneo la Omukajunguti, Mkoani Kagera ili kuwezesha ndege kubwa ziweze kuruka na kutua.

Mheshimiwa Naibu Spika, Uthamini wa awali kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi watakaoathirika na utekelezaji wa mradi ulishafanyika. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kuanza kwa ujenzi wa kiwanja hicho cha ndege. Ahsante.