Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, kuna athari gani za kijamii kwa watumishi wenza kuishi mbali na watoto wao?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Serikali amefafanua vizuri kabisa madhara yanayotokana na wenza kutokuwa pamoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu, ukiangalia athari ambazo zinatokana na wenza kutokupata nafasi ya kufanya kazi wakiwa wako pamoja, ni kubwa sana na zinaathiri jamii; na sisi tunajua kwamba familia bora ndiyo inajenga jamii bora. (Makofi)

Sasa ni nini mkakati wa Serikali wa kukabiriana na hili suala lililopo mbele yetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, je, ni nini kauli ya Serikali kwa waajiri wale ambao hawatoi fursa ya kuhakikisha kwamba wafanyakazi wao wanapata haki ya kufanya kazi wakiwa karibu na wenza wao?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zainab kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza linahusu madhara ambayo yanawapata watoto wakati wenza wao mbalimbali. Serikali kupitia MTAKUWWA imeunda Kamati Maalum za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake kwa ngazi zote. Maafisa wetu wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii wanapita kuelimisha kwa njia za vyombo vya habari, mikutano na makongamano mbalimbali pamoja na midahalo ya kitaifa ambayo inaendelea kila mkoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, nini tamko la Serikali kuhusu wenza ambao wanakatazwa kuwafuata wenza wao walipo. Kanuni na sheria zipo ambazo zinaeleza kila kitu katika Serikali. Serikali yetu imeunda sera, kanuni na miongozo ambayo inawaelemisha wananchi kufuata sheria zitakazowafanya wapate vibali vya kwenda kukaa na wenza wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelezo zaidi napenda kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge tujifunze kukaa na watoto wetu wakati wowote ule kuwapa muda maalum ambao tunaweza kuwaelimisha elimu ambayo Serikali yetu na utamaduni wetu. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake ambayo yameonesha msingi wa hoja hii muhimu sana ya kuhakikisha kwamba ustawi wa familia kwa maana ya wenza na watoto kuishi pamoja ili kuweka makuzi bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilihakikishie Bunge lako tukufu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inadhamana ya kuangalia ustawi wa watumishi wote nchini. Baada ya kutambua tatizo hili la wenza kukaa maeneo tofauti tofauti na kusababisha kuwa na athari kubwa katika malezi ya familia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ameshatoa Waraka Namba 452501 kifungu cha 6(b) kimetoa masharti ya kumhakikishia mtumishi ana uwezo wa kuomba kibali cha kuhamia kwa mwenza wake endapo eneo husika litakuwa na nafasi na atakuwa na uthibitisho wa vyeti vya ndoa na nyaraka nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nitoe wito kwa waajiri wote kuhakikisha wanazingatia kifungu cha waraka huo ili kusaidia ustawi wa familia, malezi ya watoto na kuhakikisha kwamba wafanyakazi wetu wanakuwa na fursa ya kuishi na wenza kwa kuzingatia taratibu na miongozo iliyowekwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. (Makofi)