Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya maabara kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari katika Jimbo la Mbozi?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Lakini Wilaya ya Mbozi ina shule za sekondari 44, Serikali imepelekea vifaa vya maabara kwenye shule za sekondari 12 tu. Sasa je, nini commitment ya Serikali katika hizi bilioni tano ambazo zimetengwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kusaidia shule ambazo katika Wilaya ya Mbozi hususan Jimbo la Mbozi ambazo hazijapata vifaa vya maabara? Naomba kuuliza.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu
Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ambalo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mbozi ni kwamba tutapeleka fedha kwa ajili ya shule za sekondari ambazo ameziainisha katika jimbo lake, zile zote ambazo zitakuwa zimemaliza maabara katika mwaka wa fedha unaokuja na zile nyingine ambazo tumeshanunua vifaa tunasubiri tu zile shule ambazo zitaleta taarifa tupeleke.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, natambua kazi njema anayoifanya katika Jimbo la Mbozi na ninajua ameji-commit kwa kiwango gani kwa wananchi wake. Kwa hiyo, nimuondoe shaka kwenye hilo.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya maabara kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari katika Jimbo la Mbozi?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini ziko sekondari 16 lakini sekondari 11 hatuna vifaa vya maabara ya sayansi.

Je, Mheshimiwa Waziri lini utapeleka vifaa hivyo ili wanafunzi waweze kujifunza vizuri?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba kama nilivyojibu katika swali la awali na swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, ni kwamba katika maeneo yote ambayo wameshamaliza ujenzi wa maabara sisi tutapeleka vifaa ikiwemo katika Jimbolake la Mbulu Vijijini. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge aondoe wasiwasi katika hilo.