Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 58 2022-04-14

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya maabara kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari katika Jimbo la Mbozi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikipeleka fedha katika shule za sekondari kwa ajili ya umaliziaji wa miundombinu mbalimbali ikiwemo maabara za masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi bilioni 5.14 kupitia Programu ya SEQUIP kwa ajili ya kununua vifaa vya maabara kwa shule 234 za Sekondari za Kata. Hata hivyo, Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na 2021/2022 imepeleka vifaa vya maabara katika shule za sekondari 1,258 nchini zilizokamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara zikiwemo shule 12 za sekondari za Wilaya ya Mbozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kugawa vifaa hivyo nchini ikiwa ni pamoja na shule za Wilaya ya Mbozi kwa kuzingatia mahitaji na upatikanaji wa fedha na wadau mbalimbali.