Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwa namna ya pekee nitoe pongezi kwa Mheshimiwa Naibu Waziri na Waziri na Wizara nzima ya Maji kwa utekelezaji wa miradi hii aliyoitaja swali lake na majibu ni mazuri sana. Hivi sasa Kata ya Nanganga, Mumburu unatekelezwa mradi wa maji wa shilingi milioni 500, Ndanda shilingi milioni 400, Chiwata mradi unaendelea shilingi milioni 500. Hata hivyo, napenda kufahamu toka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, wakati wa usanifu wa miradi ya Kata ya Mpanyani alipokuja Katibu Mkuu tulikubaliana kwamba Kijiji cha Mraushi patawekwa tenki. Je, ni lini kazi ya ujenzi wa tenki Kijiji cha Mraushi itaanza kufanyika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kati ya Mwena na Liloya kuna mradi unaoendelea. Kwa bahati mbaya sana mradi huu unafanya kazi vizuri sana wakati wa mvua na wakati wa kiangazi haufanyi kazi vizuri, unahitaji tena kufanyiwa marekebisho. Je, ni lini Serikali itakwenda kuufanyia marekebisho Mradi wa Liloya-Mwena? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nipokee pongezi, nafahamu anayeshukuru anaomba tena, tutarudi Ndanda tutaendelea kufanya kazi pamoja Mheshimiwa Mbunge na nampongeza Mbunge kwa uwajibikaji wake mzuri.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa tenki tunautarajia ndani ya mwaka wa fedha 2022/2023 uweze kukamilika. Vile vile katika ule mradi ambao tayari unatoa huduma japo maji kidogo yana chumvi na wakati wa kiangazi inaleta shida, Mheshimiwa Mbunge hili tumeshaliongea mara nyingi, amefika ofisini na sisi tayari tumeshalifanyia kazi, tumeshatoa maagizo pale Mtwara. Kwa hiyo, litaendelea kuangaliwa kwa jicho la kipekee kuhakikisha wananchi wanakwenda kupata maji safi, salama na ya kutosha. (Makofi)

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Shule nyingi za sekondari na primary Mkoani Mara hazina miundombinu ya maji. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha miundombinu hiyo inawafikia ili kuepuka magonjwa ya milipuko? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ghati Chomete, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Ghati amekuwa ni mlezi mzuri sana wa watoto mashuleni na amefuatilia sana hili suala la huduma ya maji mashuleni. Naomba nitumie Bunge lako Tukufu kuwaagiza Viongozi wa Mkoa wa Mara kwa maana ya MD na RM wahakikishe wanapeleka maji mashuleni, hili tulishaagiza, ni ufuatiliaji na utekelezaji tu, hivyo waweze kufanya kuanzia sasa na mwaka ujao wa fedha. (Makofi)

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba, katika mji wetu wa Tarime Mjini tunacho chanzo cha Nyandurumo ambacho ndicho kinacholisha maji katika Mji wetu wa Tarime, lakini Nyandurumo hii ipo katika Kata ya Kenyamanyori. Wakazi wa Kenyamanyori hawana maji.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba, wakazi wa Kenyamanyori wanapata maji ili waweze kutunza chanzo hiki ambacho ni muhimu sana katika Mji wetu wa Tarime? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, Spika ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael, Mbunge wa Tarime, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nampongea Mheshimiwa Michael, alishaniona katika hili. Sera ya Maji inataka vijiji vyote vilivyopo katika eneo la chanzo wawe wanufaika namba moja. Naendelea kutoa maagizo kwa MD na RMs waweze kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao. Tunakwenda kuhakikisha watu wote wanaopitiwa na mtandao wa bomba wananufaika na maji.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Supplementary Question 4

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Kata ya Kazuramimba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi yote ambayo ipo kwenye utekelezaji, tunaendelea kwa kasi nzuri sana kuhakikisha inaisha ndani ya wakati. Mheshimiwa Mbunge kama tulivyozungumza, tutasimama kwa pamoja kuhakikisha mradi huu unaisha ndani ya wakati. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Katika Kata ya Mbezi Juu, Mtaa wa Mbezi Mtoni na Sakuveda kuna changamoto kubwa ya maji. Ni lini Serikali itapeleka miundombinu hii ili wananchi waweze kupata huduma hii? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felista Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi lengo letu ni kuona tunatua akinamama ndoo kichwani na Mheshimiwa Felista amefuatilia hili, ameshaongea nami. Kama tulivyozungumza, mantahofu, haya maeneo yote maji yatapelekwa na tunataka kuhakikisha ukifika mwaka 2025 maeneo yote ya vijijini yatapata maji kwa asilimia 85 na asilimia 95 kwa maeneo ya mijini. (Makofi)