Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 72 2022-04-19

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Namajani, Mpanyani, Mlingula, Msikisi na Chingulungulu (Kata ni Namalutwe) zilizopo katika Jimbo la Ndanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mlingula ina Vijiji vitano vyenye huduma ya maji ambavyo ni Mlingula, Chikoweti na Nambaya. Aidha, katika kuboresha huduma ya maji kwenye Kata hiyo vijiji vya Namichi na Masikunyingi vinapata huduma ya maji kupitia bomba kuu linalopeleka maji kwenye maeneo yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (NAWASA). Kazi ya usanifu wa miundombinu ya maji itakamilika mwezi Juni, 2022 na ujenzi utafanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, Kata za Namajani zina vijiji vitano ambavyo vinapata huduma ya maji ni Namahinga, Ngalole, Namajani. Kata ya Mpanyani ina vijiji vitano ambapo Vijiji vya Muungano Nambawala A na Nambawala B vinapata huduma ya maji. Kata ya Nsikisi ina vijiji vitatu ambapo Kijiji cha Namalembo kinapata huduma ya maji. Vile vile katika Kata ya Namalutwe pale pameandikwa Chingulugulu, naomba isomeke Namalutwe kwa sababu Chingulugulu ni kijiji na Kijiji cha Chingulugulu kina huduma ya maji. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kazi ya utafiti wa maji chini ya ardhi imekamilika katika vijiji nane katika Kata hizo nne na uchimbaji wa visima unaendelea na miundombinu ya maji itafanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023.