Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, ni lini miradi ya umwagiliaji katika Vijiji vya Nyamterela na Katunguru pamoja na Vijiji vya Kwinda na Isole itakamilika Wilayani Sengerema?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Ni kwamba Sengerema inazo skimu Tano, katika hizi skimu Tano skimu Mbili ndiyo zimepata fedha. Sasa, nataka kupata majibu ya Serikali skimu Tatu zilizobakia; Je, lini zitapata fedha kwa ajili ya kufanya usanifu?

Swali la pili, Sengerema tunao Ushirika wetu wa Nyanza ambako kuna viwanda vitatu viko katika Wilaya ya Sengerema. Hatujawahi ku-gin pamba leo ni miaka 20.

Je, Wizara ina mpango gani kuhusiana na Ushirika katika Wilaya ya Sengerema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumwambia Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Sengerema kwamba mwaka ujao wa fedha tunajenga skimu mbili katika Wilaya ya Sengerema. Vilevile, tutatenga fedha zaidi ya Shilingi Milioni 300 kwa ajili ya kufanya usanifu kwenye skimu zilizobaki, ambazo zitatengewa fedha mwaka unaofuatia. Kwa sababu, hatuwezi kujenga skimu zote tano, kwa wakati mmoja. Kuhusu suala la Ushirika nataka nitumie nafasi hii na ninapongeza baadhi ya Vyama vya Ushirika katika nchi yetu ambavyo vimeweza kufufua ginneries. Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza kwa mwaka huu tumekubaliana Nyanza na Tanzania Agricultural Development Bank na sasa hivi ninavyoongea TADB wanafanya survey Nyanza, wanafanya survey SIMCU, wanafanya survey SHIRECU kwa ajili ya kufufua ginnery za vyama hivi vitatu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeona kwamba mfumo huu wa kuwa na ginnery zinazomilikiwa na Vyama vya Ushirika na Vyama vya Ushirika kuwa na kampuni zao narudia. Vyama vya Ushirika kuwa na kampuni zao ambazo zinaingia kwenda kununua pamba kuongeza ushindani inamsaidia mkulima.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, baada ya survey ya TADB katika ginnery za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza, tutakutaarifu kwamba ni ginnery gani ya Nyanza inafufuliwa sasa hivi. (Makofi)