Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa mradi wa umeme wa upepo Singida utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu kwamba nasikitishwa na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Spika, mradi huu toka mwaka 2016 Mheshimiwa Waziri aliekuwepo alisema 2017 utekelezaji utaanza na utakamilika 2019 leo tunaambiwa mpaka 2027, nataka kujua sababu kubwa ya mradi huu kusuasua na hizi danadana inatokana na nini?

Swali la pili, najua kwamba kulikuwa kuna majadiliano kati ya Serikali na Benki ya Exim ya China kwa ajili ya mkopo wa Dola Milioni 132. Nataka kujua majadiliano haya yamefikia wapi ili mradi huu uweze kutekelezwa na wananchi wa Mkoa wa Singida tumechoka kudanganywa. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Jesca kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimetaja miradi mitatu iliyopo katika Mkoa wa Singida sasa sijui alitaka kujua upi kati ya hiyo lakini kwa swali la pili ninaamini alitaka kujua mradi ambao unatekelezwa kati ya Mkandarasi anayeitwa GEO Wind ambaye kwa sasa financier wake ni Green Climate Fund.

Mheshimiwa Spika, miradi hii kama tulivyosema inatekelezwa na wawekezaji binafsi, Serikali tunaweka mazingira ya uwekezaji baada ya hapo yeye anatakiwa atafute mfadhili atakayeweza kumfadhili na kukamilisha eneo lake la uwekezaji.

Mheshimiwa Spika, mwenzetu wa GEO Wind huyu ni mfadhili wake wa tatu, alienda Exim wakajadiliana lakini hawakukubaliana baadaye akapata mtu mmoja anaitwa Aplonia kutoka Hispania wakajadiliana hawakukubaliana, sasa saa hizi yupo na huyo ambaye tunamuita Green Climate Fund wanaendelea na majadiliano, watakapokamilisha na wakawa tayari kuwekeza upande wetu tumeshakamilisha, tumeshaweka masharti na tuko tayari kumpokea kwa ajili ya uwekezaji.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana tukasema tunatarajia kati ya mwaka 2023 mpaka 2027 miradi hii itakuwa imekamilika baada ya kukamilisha upande wao.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa mradi wa umeme wa upepo Singida utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nami niungane na Dada yangu Jesca Kishoa jambo hili limekuwa la muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, nataka nimwombe Mheshimiwa Waziri kama atakuwa tayari yeye pamoja na hao wawekezaji GEO Wind na wengine tukutane kwa pamoja kabla Bunge hili halijaisha ili kuweza kujadili mstakabali wa mradi huu wa umeme wa upepo pale Singida Mjini? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sima la nyongeza kwamba Wizara tuko tayari kufanya jambo hilo kwa maslahi ya wananchi wa Singida na Watanzania kwa ujumla.