Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 52 2022-04-13

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa mradi wa umeme wa upepo Singida utaanza?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO imekuwa ikifanya jitihada za kuendeleza miradi mbalimbali ya kufua umeme nchini, ikiwemo miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia nishati jadidifu ya upepo katika maeneo ya Mkoa wa Singida inayotekelezwa na wawekezaji binafsi wenye nia ya kuzalisha umeme na kuiuzia TANESCO.

Mheshimiwa Spika, miradi hiyo ni pamoja na mradi wa upepo MW 50 unaotekelezwa na Kampuni ya Upepo Energy eneo la Msikii Halmashauri ya Singida Vijijini, ambapo majadiliano ya mkataba wa kuuziana umeme (Power Purchase Agreement) kati yake na TANESCO yanaendelea. MW 300 unaotekelezwa na Kampuni ya GEO Wind eneo la Kititimo Halmashauri ya Singida Mjini ambapo majadiliano baina ya Mwekezaji na Mfadhili Green Climate Fund (GCF) yanaendelea. Pia MW 100 unaotekelezwa kwa ubia wa TANESCO na kampuni ya Abu-Dhabi (Masdar) eneo la Ikungi, Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ambapo Upembuzi Yakinifu unaendelea.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi hii inatarajiwa kukamilika kati ya mwaka 2023 na 2027.