Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Je, Serikali haioni haja ya kuimarisha mawasiliano hususan kwenye Wilaya za Mipakani kama Longido na Ngorongoro ambazo bado zina mawasiliano hafifu na muda mwingine wanatumia mawasiliano ya nchi jirani?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, Arusha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna mradi wa Special Zone and Borders ambao tayari unaendelea katika utekelezaji wake, labda tutajiridhisha katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge amesema. Tutatuma wataalam wetu kwenda kuangalia kama halipo ndani ya mpango unaoendelea wa utekelezaji wa miradi ya Special Zone and Borders. Ahsante sana.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naomba kujua ni lini Wizara itajenga minara katika Kata ya Kikonda, Kinampundu na Mwangeza, ukizingatia Mwangeza wanavamiwa na tembo kila wakati, kwa hiyo wanahitaji mawasiliano kwa ajili ya kuomba msaada? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimesema hapa awali katika majibu yangu ya msingi ni kwamba kuna miradi mbalimbali inayoendelea. Niwaombe Wabunge, kuna miradi 763 ambayo imeshaletwa Bungeni, lakini pia tuna hayo maeneo ambayo ni 216 ambayo yameshafanyiwa tathmini.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliombe Bunge lako Tukufu, wajaribu kupitia katika ile miradi pale ambapo Mheshimiwa Mbunge atagundua kwamba maeneo anayoyasema bado hayajaingizwa katika mpango wa utekelezaji, basi Serikali tutayapokea kwa ajili ya kufanya hatua stahiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Waziri Kata ya Kinyamsindo, Lahoda pamoja na Sanzawa zilishafanyiwa tathmini kwa ajili ya kujengewa minara. Je, ni lini sasa wataziingiza kata hizi kwenye zabuni ili zitangazwe na hatimaye wananchi wetu waweze kupata mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Kunti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa tuna miradi ambayo inaendelea na pili kuna miradi 763 ambayo tayari Serikali imeshatangza zabuni, lakini vile vile tuna vijiji 216 ambavyo Serikali tayari imeshavifanyia tathmini. Kwa hiyo, tunaamini kwamba kwa kadri fedha itakapokuwa inapatikana, tunaamini kwamba vijiji hivyo, ikiwa pamoja na kata hiyo itaingizwa katika utekelezaji ili kuhakikisha kwamba Ilani ya Chama cha Mapinduzi ianendelea kutekelezwa kwa niaba ya Rais wa Tanzania. Ahsante sana.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ujenzi wa Mnara katika Kata ya Itetemia uliokuwa umeanza umesimama kwa takribani miezi mitatu sasa, hakuna mwendelezo wowote. Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ujenzi wa mnara huo ili wananchi wa Kata ya Itetemia waweze kupata mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa, Mbunge wa Tabora, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Itetemia na eneo la Itetemia, mradi unaojengwa pale unajengwa na kampuni ya Halotel na kwa sababu tulikuwa na changamoto ya vifaa ambavyo vilikuwa vimeletwa lakini vilikuwa vime-miss baadhi ya vipuri. Tumehakikishiwa kwamba vipuri sasa vipo njiani na pindi vitakapofika Kata hii ya Itetemia na mnara wake wa Halotel utakuwa kamili na utawashwa kwa ajili ya matumizi ya wananchi. Ahsante sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 5

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano katika Vijiji vya Katesh, Endagulda pamoja na Yaeda Jimbo la Mbulu Vijijini? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Katesh, Endagulda pamoja na Hhayeda ambayo yanatoka katika Jimbo la Mheshimiwa Flatei Massay, kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Asia Halamga kwa kazi kubwa ambayo ameendelea kufuatilia katika Mkoa wa Manyara, kuhakikisha kwamba huduma ya mawasiliano inaimarishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, maeneo yote haya yote matatu ambayo ameyataja Mheshimiwa Asia Halamga tayari tumeyaingiza katika mradi wetu wa minara 763.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 6

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa kuiweka Kata ya Ikindwa kwenye mpango wa kujenga mnara katika zabuni iliyopitishwa mwezi Oktoba, lakini nina swali la nyongeza kuhusu Kata ya Karitu. Miaka miwili, mitatu iliyopita, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ulifanya tathmini kwenye Kata hii ya Karitu na ukabaini kuna upungufu wa mawasiliano na ukaingizwa kwenye zabuni. Je, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba kinachotakiwa kufanywa ni kutangaza upya, kuingiza upya Kata hii ya Karitu kwenye zabuni, badala ya kwenda kufanya tathmini upya kwa sababu kazi ya tathmini ilishafanyika na ndio maana kata hii iliingizwa kwenye zabuni miaka miwili, mitatu iliyopita? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Serikali ilifanya tathmini katika maeneo haya, lakini kulingana na uwekezaji mbalimbali wa makampuni ambayo ni tofauti kabisa na uwekezaji wa Serikali, inawezekana kabisa mahitaji yanayohusika yanaweza kubadilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hivyo, kama nilivyojibu katika swali la msingi ni kwamba maeneo ambayo yalikuwa yameshafanyiwa tathmini katika Jimbo la Bukene yalikuwa ni mengi lakini tunaenda hatua kwa hatua kulingana na upatikanaji wa fedha. Tayari Kata ya Ikindo imeshaingizwa katika mradi ambao umeshatangazwa tarehe 22 Oktoba. Tunaamini kwamba kulingana na fedha zinavyozidi kupatikana basi na hii Kata ya Karitu na yenyewe itaingizwa katika utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 7

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Kata ya Nyaruhande, Shigala, Wilaya ya Busega hazina minara ya mawasiliano, je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano katika kata hizo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Mkoa wa Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Nyarukande tayari imeingizwa katika utekelezwaji wa miradi 763. Kwa hiyo tuombe tu kwamba utaratibu utakapofika katika maeneo hayo, basi wananchi waandaliwe kwa ajili ya kutoa maeno kwa ajili ya ujenzi wa minara hiyo. Ahsante sana.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nina swali moja; je, ni lini Serikali itaweka minara ya mawasiliano kati ya Manyoni na Tabora?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Genzabuke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba eneo la Manyoni - Tabora bado lina changamoto ya mawasiliano na kwa sababu tunatekeleza kwa kadri fedha inavyopatikana, tunaamini kabisa kwamba katika eneo hili, tunalichukua na tunahakikisha kwamba tunaenda kulifanyia tathmini na tuangalie upana wa tatizo jinsi lilivyo ili tukachukue hatua ya kuhakikisha kwamba mawasiliano katika eneo hilo yanapatikana.

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 9

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Mamba Kusini iliyopo katika Jimbo la Vunjo, kuna shida kubwa ya mawasiliano.

Je, ni lini Serikali inaweza kurekebisha tatizo hili? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kupokea changamoto ya mawasiliano katika Kata ya Vunjo ili tukaifanyie tathmini ili sasa tuweze kufikisha mawasiliano katika eneo hilo. Ahsante sana.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Supplementary Question 10

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Pamoja na juhudi nzuri za Serikali za kujenga minara, badala ya kuijaza Tanzania na utitiri wa minara, ni lini sasa itakuja na teknolojia ya kutumia mnara mmoja ili kuepusha nchi nzima kuwa na utitiri wa minara? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Askofu, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari teknolojia ya kutumia mnara mmoja inatumika hapa nchini. Tunaita core location, core location maana yake kwamba Tigo inakuwepo pale pale, Airtel inakuwepo pale pale, Voda inakuwepo pale pale, kampuni zote zinakuwepo pale pale. Changamoto inayokuwepo ni katika maslahi ya hizo kampuni wanapo- share wanaona kama vile wananyang’anyana wateja. Kwa hiyo, hii ni changamoto ambayo inawahusu mobile network operator moja kwa moja, ambapo wao ndio wanaweza kuamua kwamba waende ku-share ama kutoku-share, kulingana na maslahi ya kibiashara zaidi. Ahsante.