Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 126 2022-11-09

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Karitu na Ikindwa – Bukene?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) iliifanyia tathmini Kata ya Ikindwa iliyopo katika Wilaya ya Nzega na kubaini kuwa ina changamoto ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya simu na hivyo kata hiyo imejumuishwa katika zabuni iliyotangazwa tarehe 24 Oktoba, 2022 kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Kata ya Karitu, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa wote itaifanyia tathmini kata hiyo ili kubaini mahitaji ya mawasiliano na kuiingiza katika zabuni zitakazotangazwa na Mfuko katika awamu zifuatazo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.