Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kata ya Itaka na Nambinzo na TFS kuhusiana na Pori la Hifadhi Isalalo?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nauliza hili swali hii ni mara ya nne, na kila ninapouliza napata majibu tofauti. Mgogoro huu hauwezi kwisha kwa Serikali kusema kwamba hakuna mgogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali la nyongeza: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutuma timu ya Maafisa wa Wizara na mimi na yeye kuongozana kwenda kule kuongea na wananchi wa Itaka na Mbinzo na wa Kata ya Isalalo kujua nini kinachoendelea kwa wananchi wale ambao kwa miaka zaidi ya 50 wamekuwa wakilitumia eneo hilo kwa shughuli zao za kilimo? Ahsante (Makofi)

NAIBU SPIKA: Sasa umeuliza mambo mawili; atume timu au aende yeye?

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, yote mawili.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Answer

NAIBU SPIKA: Aje yeye, nafikiri ndiyo muhimu. Mheshimiwa Waziri utaambatana naye.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kata ya Itaka na Nambinzo na TFS kuhusiana na Pori la Hifadhi Isalalo?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Nimesikia majibu ya msingi ya swali hili. Kwanza naomba kabisa kabla sijauliza swali; Mheshimiwa Waziri tunaomba ufanye ziara kwenye vijiji vyetu ili hayo matamko ambayo wewe unayatoa hapa uweze kuwaambia wananchi wenyewe wasikie kama sehemu ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu: Je, ni lini Serikali itavimegea nafasi za kulima wananchi wa Itumbula, Ivuna, Mlomba, Itelefya pamoja na maeneo mengine yote ambayo yapo ndani ya Jimbo la Momba ambayo yanahitaji kumegwa kupata maeneo ya kulima kwa sababu maeneo yao yote yamezungukwa na hifadhi na maeneo hayo wananchi wenyewe walitoa kwa Serikali kwa ajili ya kulinda misitu; na sasa hivi wamezaliana? Wataenda wapi ili waweze kulima na kuendeleza shughuli zao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni kulinda meneo yaliyohifadhiwa. Kama kuna ombi la wananchi kumegewa, basi walete maombi hayo yataangaliwa, lakini pia na sisi tutaangalia kama maeneo hayo yana vyanzo vya maji, yana shughuli ambazo zinapaswa kuhifadhiwa vizuri, basi tutawataarifu wananchi namna iliyo bora.