Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 123 2022-11-09

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kata ya Itaka na Nambinzo na TFS kuhusiana na Pori la Hifadhi Isalalo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) haina mgogoro wowote wa mpaka kati ya msitu wa Isalalo-Lunga na wananchi wa Kata ya Itaka na Nambinzo. Hali iliyopo ni uvamizi unaofanywa na wananchi wachache wanaoingia kwenye hifadhi kinyume cha sheria kwa ajili ya kilimo cha mazao ya muda mfupi. Aidha, ndani ya msitu huu hakuna makazi na Wizara imeendelea kuimarisha mipaka ya msitu kwa kuweka vigingi vikubwa 20 na vinavyoonekana vizuri. Sambamba na hilo, mabango 15 yamewekwa ili kuwakumbusha wananchi kuzingatia sheria.