Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Ndaki ya Sayansi ya Afya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Mamlaka ya Mji wa Mbalizi?

Supplementary Question 1

MHE. ORANI M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kwanza kuipongeza Serikali kwa kuanzisha na vile vile kuboresha hii ndaki ya afya ikiwa sehemu ya uboreshaji wa Afya nchini kwetu. Sasa kwa vile kuna ongezeko kubwa sasa hivi la magonjwa yasiyoambukizwa: Je, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na hii ndaki ya afya wamejiandaa vipi kukabiliana na hilo ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa hiki chuo kinaonekana kuwa kitakuwa na eneo kubwa sana, kwa hiyo, kinategemea kuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi.

Je, kitakuwa na wanafunzi wangapi na pia wafanyakazi wangapi mara kitakapokamilika kujengwa? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kawaida kwenye vyuo vyetu vikuu, jukumu lao la kwanza ni kuhakikisha kwamba utoaji wa taaluma ya aina mbalimbali au katika maeneo ambayo yanakuwa yameainishwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kwamba chuo chetu cha tiba ya binadamu Muhimbili kinaendelea kufanya utafiti wa magonjwa haya yasiyoambukizwa kwa undani zaidi ili kujua chanzo cha magonjwa haya na namna gani tunaweza kuyaepuka. Kwa hiyo, nimwondooe wasiwasi, na mikakati yetu kama Serikali na kama Wizara ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kufanya tafiti hizo za kina.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili ni kuhakisha tunatoa elimu kwa Umma kuhusu namna gani ya kuepuka na kujikinga na magonjwa haya yasiyoambukiza. Kwa hiyo, hilo litakuwa ni jukumu la pili na mkakati wetu wa pili. Eneo la tatu ni kubadili sasa mifumo ya maisha yetu tuliyozoea kuishi ili kuweza kuepukana na magonjwa haya kama vile kubadili milo yetu na kuendelea kufanya mazoezi ya kila siku. Kwa hiyo, hiyo ndiyo mikakati yetu na tutahakikisha kwamba chuo kinaenda ku-emphasize kwenye mikakati ili kuhakikisha kwamba mambo haya yanakaa sawa sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili linahusiana na suala la takwimu. Ameulizia wanafunzi watakuwa wangapi katika ndaki hii pamoja na watumishi watakuwa wangapi? Kwa vile sasa takwimu hizo sina hapa, naomba Mheshimiwa Mbunge aridhie kwamba tukimaliza Bunge hili tuweze kutafuta takwimu hizi na niweze kumpatia rasmi. Nakushukuru sana.