Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati reli ya TAZARA?

Supplementary Question 1

MHE. DEOGRATIUS P. MWANYIKA : Mheshimiwa Naibu spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri. Pamoja na uwekezaji anaouongelea wa bilioni 13 changamoto kubwa ya reli ya TAZARA ni kwamba hata ukiwekeza hizo fedha, uendeshaji kibiashara ni tatizo. Sasa Serikali ina mpango gani wa muda mfupi ili reli hii iendeshwe kibiashara iondoe maroli mengi ambayo yako barabarani badala ya kutumia mzigo uende kwa treni?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tuliambiwa hapa na kulikuwa na ushauri wa Kamati ya Bajeti, kwamba mkataba wa uwekezaji wa Reli ya TAZARA ndilo moja ya tatizo kubwa sana linalotufanya tusiweze kuitengeneza reli hii vizuri. Sasa swali, Serikali ina mpango gani na imechukua hatua gani mpaka muda huu kurekebisha mkataba huo au kuu-terminate kabisa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa ujenzi na uchukuzi napenda kujibu Maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwanyika kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala hili la Reli ya TAZARA, pamoja na Wabunge wote wa Nyanda za Juu Kusini wamekuwa kila mara wakifuatilia jambo hili. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini, mpango wa muda mfupi ndio huo ambao tumetenga fedha kiasi cha Shilingi bilioni 13.1 na tutafanya manunuzi ambayo nimejibu kwenye jibu langu la Msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Mkataba, mkataba ama Sheria Namba 4 ya mwaka 1995 ya TAZARA ndiyo ambayo inakwamisha tusiendelee hasa katika uwekekezaji kama nchi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zambia walipokutana walielekeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tukutane na wenzetu wa Zambia. Mikutano hii imefanyika mwezi uliopita tarehe 14/10/2022 mpaka tarehe 15/11/2022 na mimi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri nilimwakilisha Lusaka Zambia kwa ajili ya kujadili Sheria hii. Mwishoni mwa Desemba tutakutana tena ili tuihuishe halafu baadae tutaileta kwenye Mabunge yote mawili ya nchi ya zambia pamoja na nchi ya Tanzania ili sasa kila nchi ipate fursa ya kuwekeza upande wake.