Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 119 2022-11-09

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati reli ya TAZARA?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya reli ya TAZARA. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 13.1 kwa ajili ya ununuzi wa mataruma ya mbao kwa ajili ya kufanyia ukarabati madaraja 172 yaliyopo upande wa Tanzania, ununuzi wa mtambo wa kisasa wa kushindilia kokoto kwenye reli, na ununuzi wa mtambo wa kuvunjia kokoto (secondary crusher) kwa ajili ya kuongeza kokoto za aina mbalimbali zinazotumika katika kufanyia matengenezo ya njia ya reli kati ya Dar es Salaam – Tunduma na Msolwa - Kidatu. Aidha, fedha hizo pia zitatumika kukarabati mabehewa 21 ya treni za abiria za Udzungwa na treni za abiria za mjini (commuter) za Jijini Dar es salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa mikakati ya muda wa kati na mrefu, Serikali za Tanzania na Zambia zimeandaa mpango wa biashara wa miaka mitano ambao unatarajiwa kupitishwa na Baraza la Mawaziri wa TAZARA mwishoni mwa Novemba, 2022. Aidha, Serikali za Tanzania, Zambia na China zimeunda timu ya pamoja kwa ajili ya kuandaa mkakati wa pamoja kwa kuishirikisha Serikali ya Watu wa China katika kugharamia maboresho ya TAZARA. Ahsante.