Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Polisi Matangatuani Wilayani ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini bado naona iko haja ya Mheshimiwa Naibu Waziri kulipa kipaumbele suala la kwenda kukiona kituo kile kwa sababu Askari wale wanafanya kazi katika mazingira magumu.

Je, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi kwenda katika eneo hilo la Kituo cha Polisi cha Matangatuani ili kuweza kutoa msukumo zaidi katika bajeti hiyo 2023/2024 kufanikisha ujenzi huo wa kituo kipya lakini pia na nyumba za makazi ya Askari Polisi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ambayo kwa kweli yanakaribia kufanana ya Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba eneo hilo halina Kituo cha Polisi lakini jambo kutia moyo wananchi hawa tayari wametenga eneo la kutosha kujenga kituo na nyumba za watumishi upande wa Polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaahidi kwamba niko tayari kukitembelea ili kuona kiasi gani kinahitajika na pia kuweka msukumo ili jengo hilo likamilishwe kwa haraka baada ya kutolewa kwa fedha hizi. Kwa hiyo, kuongozana naye wala halina tatizo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Polisi Matangatuani Wilayani ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kituo cha Polisi kilichopo wilaya ya Mkoani mkoa wa Kusini Pemba kipo katika hali mbaya.

Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati kituo hicho japo kwa dharura?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Mwinyi Kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba maeneo ya Pemba vituo vyake vingi vya Polisi vimechakaa vinahitaji kufanyiwa marekebisho au kiujengwa vipya. Tumeanza na majengo ya Kamanda wa Polisi wa mikoa miwili ya Pemba, lakini tutaendelea kujenga hivi vya ngazi ya wilaya na vingine vidogo ili hatimaye maeneo yote yaweze kupata vituo vinavyostahiki. Nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ziara nitakayoifanya huko Pemba, moja ya maeneo ni kuzingatia maeneo haya ambayo hayana kabisa vituo vya Polisi ili na wao waweze kupatiwa vituo hivi kwa ajili ya usalama wa raia na mali zao.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Polisi Matangatuani Wilayani ya Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati maeneo mengine wanazungumzia habari ya ukarabati wa vituo vya Polisi, kwenye Mkoa wetu wa Iringa katika wilaya ya Kilolo bado Serikali haijajenga Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ngazi ya wilaya ilhali ni zaidi ya miaka ishirini sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi.

Je, ni lini sasa Serikali itajenga makao makuu ya polisi Wilaya ya Kilolo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yaliyotangulia, ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba wilaya zote zinapata vituo vya polisi vyenye hadhi ya wilaya. Hivyo kutokana na upatikanaji wa fedha tunakwenda kwa awamu. Nimuahidi tu Mheshimiwa Ritta kwamba Wilaya ya Kilolo ni miongoni mwa wilaya zitakazozingatiwa hasa ukizingatia kwamba kuna uharibifu mkubwa wa mazingira yanayohitaji usimamizi wa sheria kwenye maeneo hayo. Kwa hiyo itapewa kipaumbele katika bajeti zetu.

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Polisi Matangatuani Wilayani ya Micheweni?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa umbali kutoka Nachingwea – Liwale ni zaidi ya Kilometa 130 na Kilwa – Liwale ni zaidi ya kilometa 260.

Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi pale Kibutuka Wilaya ya Liwale na Njinjo kule Wilaya ya Kilwa? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Ungele kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa umbali alioutaja Mheshimiwa Mbunge kwamba kutoka eneo moja hadi kituo cha Polisi ni zaidi ya kilometa 100 ina-justify kabisa umuhimu wa uwepo wa kituo cha Polisi. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba tutaelekeza Kamanda wa Polisi Mkoa na Jeshi la Polisi kwa ujumla wake kufanya tathimini ya uhitaji wa kituo cha Polisi maeneo hayo uliyoyarejea ili mpango wa ujenzi wa vituo hivyo uweze kutekelezwa. Ahsante sana.