Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 116 2022-11-09

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Polisi Matangatuani Wilayani ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi cha Matangatuani kilichopo Wilaya ya Micheweni ni kituo kilichojengwa siku nyingi na jengo lake ni chakavu. Katika tathmini iliyofanyika jengo hilo halifai kufanyiwa ukarabati kutokana na udhaifu wa kuta za jengo hilo. Serikali ina mpango wa kujenga Kituo kipya cha Polisi cha daraja "C". Michoro na makadirio yameshafanyika na kiasi cha Shilingi 427,604,929 kinahitajika kwa ajili ya kujenga Jengo la Kituo pamoja na nyumba mbili za makazi ya Askari. Fedha za ujenzi zinatarajiwa kuombwa kwenye Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 kutegemea na upatikanaji wa fedha.