Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DAVID C. CHUMI aliuliza: - Je, Serikali inakusanya kiasi gani cha asilimia Tano ya zawadi ya washindi wa mchezo wa kubashiri na kimechangia kiasi gani kukuza michezo?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID C. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na ninakuomba kwa ridhaa yako kabla ya maswali yangu mawili ya nyongeza nitumie nafasi hii kuwapongeza Serengeti Girls na Tembo Warriors kwa kufika hatua ya robo fainali, lakini pia kuwapongeza Simba Queens ambao leo wanacheza hatua ya nusu fainali na Mamelodi Sundowns na kuwapongeza Simba kuingia hatua ya makundi na kuwaombea Yanga leo dhidi ya Club Africain waweze kushinda na kuingia hatua ya makundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo nina maswali mawili ya nyongeza. Je, Serikali iko tayari kuona kwamba sehemu ya fedha hizi inatumika pia katika kuboresha mchezo wa riadha ambao unaweza kutusaidia katika kujitangaza kwa umadhubuti katika kushiriki michezo kama vile Tokyo Marathon, New York Marathon, Bostin Marathon na kadhalika?

Swali la pili, kwa muda mrefu mojawapo ya shida katika michezo yetu hasa mchezo wa soka ni kiwango duni cha waamuzi.

Je, Serikali iko tayari kutenga sehemu ya fedha hizi kufanya mafunzo maalum kwa ajili ya waamuzi ili waamuzi wetu kuwajengea uwezo na hivyo kuwawezesha kushiriki katika kuchezesha michezo ya AFCON, World Cup na kadhalika? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza Mheshimiwa Chumi amependa kufahamu kama Serikali ipo tayari sasa kutenga sehemu ya fedha hizi kuhakikisha pia wanaweza ku-support riadha. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba sisi kama Wizara tunayo michezo Sita ya kipaumbele ikiwemo riadha. Kwa hiyo, tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ku-support riadha ili iendelee kufanya vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, amependa kufahamu kama fedha hizi pia zitatumika katika kuwezesha waamuzi. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu na Watanzania pia kwamba chini ya BMT wameendelea kusimamia kwamba vyama vya michezo waweze kuwaandaa waamuzi. Na niwapongeze TFF wiki hii iliyopita walikuwa na programu ya vijana 30 pale Uwanja wa Taifa wakishirikiana na FIFA kuhakikisha kwamba tunapata waamuzi kwenye michezo hii. Ahsante. (Makofi)