Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 114 2022-11-09

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DAVID C. CHUMI aliuliza: -

Je, Serikali inakusanya kiasi gani cha asilimia Tano ya zawadi ya washindi wa mchezo wa kubashiri na kimechangia kiasi gani kukuza michezo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa David Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 mpaka mwezi Septemba mwaka 2022, Wizara imepokea kiasi cha Shilingi za Tanzania Bilioni 3.4 ikiwa ni asilimia Tano ya mapato yatokanayo na michezo ya kubashiri. Kwa mujibu wa muongozo wa mfuko wa Maendeleo ya Michezo fedha hizi hutumika kuhudumia Timu za Taifa, kutoa mafunzo kwa wataalamu wa michezo na wanamichezo, kuibua na kuendeleza vipaji vya michezo pamoja na kujenga na kukarabati miundombinu ya michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Timu za Tembo Warriors na Serengeti Girls ni miongoni mwa wanufaika wa hivi karibuni wa fedha hizo katika maandalizi na ushiriki wao kwenye mashindano ya Kombe la Dunia la mpira wa miguu kwa Walemavu na Wanawake chini ya miaka 17 ambapo zilifanikiwa kufika hatua ya robo fainali na kuipandisha daraja nchi yetu katika nafasi za soka Duniani. Ahsante.