Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufikisha mbegu za Soya kwa Wakulima wa Jimbo la Newala Vijijini hasa katika Kata za Tarafa ya Chilangala?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Je, Serikali imejipangaje kuhusu masoko ya ndani na nje ya nchi ili wakulima walime wakijua kwamba masoko watapata baada ya mazao kuvunwa?

Swali la Pili, kwa kuwa hali ya hewa ya Tarafa ya Chilangala, kwa leo hii imebadilika siyo kama ile miaka ya 1970 na 1980 wakati zao hili linalimwa. Je, Serikali imejipangaje kwenda kutoa elimu kwa wakulima hawa ili waweze kulima kilimo chenye tija? Ahsante.(Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hali ya hewa na mabadiliko ya tabianchi, Wizara kupitia TARI - Naliendele na Mlingano, sasa hivi wanafanya mapping ya soil na kuweza kutoa elimu kwa wakulima kutokana na ekolojia ya maeneo husika na hili zoezi ni on going, tutakapoanza program ya soya katika Mikoa ya Kusini, TARI Naliendele moja ya jukumu lao la msingi itakuwa ni kutoa elimu kwa wakulima ili tuweze kupata tija, na ndiyo maana tunaanza eneo dogo la Wilaya ya Newala Vijijini and then baada ya hapo mwaka unaofuata wa 2023/2024 kulifanya hili zao kuwa ni zao la tatu katika Mikoa ya Kusini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu masoko changamoto masoko ipo hasa kwa mazao ambayo siyo ya msingi ya chakula kwa binadamu, kama mazao ya korosho na mazao mengine. Kwa hiyo, hatua ambayo tunaifanya kama Serikali sasa hivi na mtaona mwaka kesho, ni Serikali kuweka nguvu kubwa katika kuongeza thamani kwa mazao ambayo tunayazalisha ndani ya nchi na kuwasaidia private sector ambao wamewekeza katika maeneo hayo kuwapa nguvu na kuwasaidia infrastructure development ili waweze kuongeza thamani katika mazao yetu na kuhakikisha kwamba tunapata zile international certification ili tuweze kumaliza hayo matatizo.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufikisha mbegu za Soya kwa Wakulima wa Jimbo la Newala Vijijini hasa katika Kata za Tarafa ya Chilangala?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi. Mheshimiwa Waziri huu ni msimu wa kilimo kwa Mkoa wa Rukwa na Nyanda za Juu Kusini lakini mpaka sasa nazungumza, upatikanaji wa mbolea na mbegu bora Wilaya ya Nkasi na Mkoa mzima wa Rukwa una changamoto.

Ni nini mkakati wa Serikali ili msiwe kikwazo kwa wakulima hawa?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Aida, nadhani jana wakati tunafanya semina aidha hakuwepo tulitoa majibu yote ya kina kuhusu hili eneo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu eneo lake, Wilaya yake, jana nimeongea na Mkuu wa Wilaya, tumeongea namna gani baadhi ya maeneo ambayo ni Tarafa zinazo wakulima wengi ziweze kufikiwa mbolea, tumeiomba Halmashauri yake iweze kutusaidia kupata usafiri ili sisi tuweze kuwasaidia mafuta waweze kusambaza mbolea maeneo ambayo mawakala hawafiki. Lakini wakala yupo Jimboni kwako na anauza mbolea. Tatizo lililopo ni mbolea kufika vijijini jambo ambalo tunashirikiana na ofisi ya Mkurugenzi na DC kwa ajili ya kufanya hivi baada ya wewe kuleta hili lalamiko kwetu. (Makofi)