Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 113 2022-11-09

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufikisha mbegu za Soya kwa Wakulima wa Jimbo la Newala Vijijini hasa katika Kata za Tarafa ya Chilangala?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijin,i kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2022/2023 Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Newala imetenga shilingi 6,000,000 za kuwezesha ununuzi wa kilo 3,000 za mbegu bora za soya. Mbegu hizo zitasambazwa kwa wakulima wa soya katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala ikiwemo Tarafa ya Chilangala.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeiwezesha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania kituo cha Utafiti (TARI) Naliendele kilo 2,260 za mbegu ya msingi ya soya itakayotumika kuzalisha tani 90 za mbegu iliyothibitishwa ubora ili kuimarisha upatikanaji wa mbegu katika Mikoa ya Kusini kwa msimu wa mwaka 2023/2024 na kulifanya zao hilo kuwa la tatu kwa wakulima wa kusini baada ya korosho, ufuta na sasa Soya.