Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza magari RUWASA – Simiyu ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini hasa magari mapya ya Wilaya zingine za Mkoa wa Simiyu yatapelekwa ili kuweza kusimamia miradi ya maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Mkoa wa Simiyu una changamoto kubwa ya vyanzo vya maji, je, RUWASA wamejipangaje, kupeleka mitambo ambayo itasaidia katika kunusuru changamoto kubwa ya maji huku tukisubiri Mradi Mkubwa wa Maji wa Ziwa Victoria?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa ameuliza lini haswa, mara baada ya magari kufika Mheshimiwa Mbunge magari yatafika sisi ni watu wa kuahidi na kutekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu vyanzo vya maji Mkoa wa Simiyu, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge, kwa Mkoa wa Simiyu tuna mradi mkubwa zaidi ya bilioni nne ambao unatekelezwa kwa mabadiliko ya tabia nchi. Kwa hiyo, Mkoa wa Simiyu tayari umeshatupiwa jicho la kipekee kabisa na tayari miradi hii imeanza kutekelezwa. Vilevile vyanzo vya maji na kwa kutumia magari haya ambayo Mheshimiwa Rais ametupatia fedha nyingi, tayari ni tarehe 11 magari yatazinduliwa na tayari utaratibu wa kufika katika mikoa mbalimbali utaendelea.