Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 111 2022-11-09

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza magari RUWASA – Simiyu ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuijengea uwezo RUWASA, Mkoa wa Simiyu ili iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya magari 37 yalinunuliwa ambapo gari moja lilikabidhiwa RUWASA, Mkoa wa Simiyu na gari nyingine ilipelekwa Wilaya ya Itilima.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika jitihada za kuendelea kuboresha mazingira ya kazi ya RUWASA nchini, Serikali itanunua jumla ya magari ya 86 kwa ajili ya RUWASA na magari hayo yatapelekwa kwenye wilaya mbalimbali nchini ikiwemo Mkoa wa Simiyu.