Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kulipatia Jeshi la Polisi magari mapya kama moja ya vitendea kazi ili litekeleze majukumu yake ipasavyo?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, naomba nimuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa mikubwa na yenye watu wengi lakini kumekuwa na changamoto kubwa sana ya usafiri kwa askari wetu katika vituo mbalimbali. Serikali inampango gani wa kupeleka magari ili kuweza kurahisisha kazi za askari wetu wanapokutana na matukio?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Jimbo la Tabora mjini lina kituo cha Central Police, lakini kumekuwa na changamoto kubwa sana, na nimekuwa nikiliuliza sana swali hili la usafiri, hata gari lililopo ni tia maji tia maji. Serikali ina mpango gani basi angalau katika bajeti hii kupeleka magari machache katika Mkoa wa Tabora, hususani Jimbo la Tabora Mjini ili kurahisisha kazi za askari wetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba kweli Mkoa wa Tabora ni mkubwa na uhitaji wake wa magari hauhitaji kupingwa, iko wazi. Kwa kulitambua hilo, Mkoa wa Tabora umepata mgao wa magari. Katika magari 78 tuliyoyapokea mwezi uliopita Tabora wamepata magari mawili. Moja limepelekwa kwa RPC Tabora na jingine limekwenda FFU Tabora. Kuhusu manispaa ya Tabora Mjini niahidi, kadri tutakapokuwa tunapata fedha, kama ambavyo mwaka huu tumetengewa Shilingi bilioni 15. Fedha zitakazopatikana tutanunua magari na Tabora kwa uhitaji wake pia watafikiriwa kupewa gari. Nashukuru.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kulipatia Jeshi la Polisi magari mapya kama moja ya vitendea kazi ili litekeleze majukumu yake ipasavyo?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwenye Bunge la Bajeti lililopita Mheshimiwa Naibu Waziri aliniahidi kupeleka fedha kwenye ujenzi wa Kituo cha Polisi kilichopo katika Halmashauri ya Ushetu; na wananchi wale walishajichanga pamoja na wadau mbalimbali wakajenga msingi. Sasa nataka nijue, ni lini Serikali inapeleka fedha hizi ili kuanza ujenzi wa Kituo cha Polisi katika Halmashauri ya Ushetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu maeneo ya Wilaya mpya kama ilivyo ya Ushetu wanahitaji kuwa na vituo vya polisi ili kusogeza huduma za usalama wa raia karibu zaidi na wananchi. Ni ahadi yetu kwamba kwa vyovyote vile kwa sababu wananchi wameshajitokeza, wamechangia nguvu zao na jitihada wakafikia mpaka kiwango cha msingi, nimtie moyo Mheshimiwa Mbunge, kwamba pale ambapo tutapata fedha kwa ajili ya ujenzi, Wilaya ya Ushetu itazingatiwa pia. Nashukuru.