Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 105 2022-11-08

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA K.n.y. MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kulipatia Jeshi la Polisi magari mapya kama moja ya vitendea kazi ili litekeleze majukumu yake ipasavyo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnesta Lambert Kaiza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kulipatia Jeshi la Polisi magari kama nyenzo ya kutendea kazi. Mkakati wa Serikali ni kutenga fedha kwenye Bajeti yake kila mwaka ili kununulia vitendea kazi muhimu yakiwemo magari na pikipiki. Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Jeshi la Polisi limetengewa kiasi cha Shilingi Bilioni 15 kwa ajili ya ununuzi wa magari 101 na pikipiki 336. Nashukuru.