Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo kikubwa cha kupozea umeme Kwambwembwele Vibaoni?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ni hatua zipi zimefikiwa katika ujenzi wa njia ya msongo wa Kilovoti 132 inayotokea Mkata kupita Handeni Mjini kwenda Kilindi?

Swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kuwa kukatikakatika kwa umeme na kutokuwa na umeme unaokidhi ndani ya Wilaya ya Handeni kumesababisha shughuli za uzalishaji kusimama na hasa kwenye migodi mikubwa iliyopo ndani ya Wilaya.

Je, uko tayari kuambatana na mimi baada ya Bunge hili ukaione hali halisi ya jinsi ambavyo uzalishaji umesimama kwenye viwanda vyetu? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua iliyofikiwa sasa katika utaratibu wa kujenga njia ya Mkata kwenda Kilindi kupitia Kwambwembwele, Handeni Mjini ipo katika utaratibu wa zabuni. Tunatarajia mwishoni mwa mwaka huu mkandarasi wa eneo hili na maeneo mengine ambapo tutajenga vituo vya kupooza umeme na line za kusafirisha umeme watakuwa wamepatikana. kwa hiyo saa hivi hatua ni ya zabuni na tayari maombi yameshafanyika inaendelea evaluation kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la pili, nipo tayari kabisa kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda Handeni Mjini lakini pia na maeneo mengine yenye matatizo ya namna hii ili tujionee na tuweze kuweka msukumo katika utekelezaji wa maelekezo na ahadi za Serikali kwa wananchi. (Makofi)